• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

MBINGA DC YAPEWA 'HEKO' USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

Tarehe ya kuwekwa: June 28th, 2021

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imepongezwa kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye maeneo mbalimbali ya Halmashauri hiyo.

Hayo yamejiri leo Juni 28, 2021 wakati wa ziara ya Kamati ya Siasa ya Wilaya, ambayo imetembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga.

Mhe. Bedda Hyera ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, CCM Wilaya ya Mbinga, Mhe. Bedda Hyera ambaye pia ameongoza Kamati hiyo amesema wao kama Chama chenye jukumu la kuisimamia Serikali wameridhishwa sana na hali ya miradi yote iliyotembelewa na Kamati hiyo.

"Sisi kama Chama cha Mapinduzi tumeridhika sana na utekelezaji wa miradi, toka tumeanza mpaka tumefika hapa unaofanywa na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga". Amesema Mhe. Hyera

Mwenyekiti huyo amesema ubora wa miradi hiyo ni matokeo ya usimamizi mzuri na hivyo kupelekea kuwa na miradi mizuri yenye ubora, tija kwa jamii na inayoendana na thamani halisi ya fedha zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo

Aidha Mwenyekiti huyo wa CCM amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Ndg. Juma Mnwele na menejimenti yake nzima kwa kusimamia kikamilifu utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri hiyo

"Mkurugenzi pamoja na wakuu wako wa Idara, sisi (CCM) hatuna cha ajabu cha kuwapa zaidi ya kuwasemea vizuri, nadhani ukimsemea mtu vizuri mungu anambariki na kumuinua zaidi ya pale alipo". Ameongeza Mwenyekiti huyo.

Kamati ya Siasa Wilaya ya Mbinga imetembelea jumla ya miradi saba ya maendeleo, ikiwa ni utaratibu wake wa kila nusu mwaka (miezi 6) wa kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo huku miradi iliyotembelea kipindi hiki ikiwa ni Shule Teule ya Sekondari ya Wavulana Mbinga (Mbinga Boys) iliyopo Kijiji cha Ndongosi, Ujenzi wa Zahanati Kijiji cha Ruanda, Kikundi cha Wanawake na Umoja wa Vijana (Ruanda) pamoja na ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa na ofisi moja Shule ya Msingi Mabuni (Kijiji cha Mabuni).

Miradi mingine iliyotembelewa ni ujenzi wa madarasa mawili, ofisi moja na matundu saba ya vyoo Shule ya Msingi Mtazamagama (Amanimakolo), ujenzi wa ofisi za Halmashauri, kikundi cha vijana cha Chipukizi na mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya, yote ikitelekezwa Kijiji cha Kigonsera

Imeandikwa na 

Salum Said,

Afisa Habari, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga.

Juni 28, 2021



Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit