• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

DC MANGOSONGO AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE MBINGA DC

Tarehe ya kuwekwa: February 9th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Aziza Mangosongo amewaongoza wajumbe wa Kamati ya Lishe ngazi ya Halmashauri wakati wa kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe kwa kipindi cha robo ya pili Oktoba hadi Disemba 2023/2024.

Kupitia kikao hicho ambacho kimefanyika Februari 9, 2024 DC Mangosongo amewaelekeza watendaji wote wa Kata na Vijiji ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kuhakikisha wanasimamia kikamilifu utekelezaji wa afua za lishe kwenye maeneo yao.

Ili kukabiliana na tatizo la lishe duni na utapiamlo kwa watoto hususani wanafunzi Mkuu huyo wa Wilaya ameagiza walimu kwa kushirikiana na jamii kuhakikisha wanafunzi kwenye shule zote za msingi na sekondari wanatumia unga wenye virutubisho.

Aidha ametoa maelekezo kwa watendaji wa kata kusimamia na kufuatilia ufungwaji wa mashine zitakazozalisha unga wenye virutibisho kwenye maeneo yao na kwamba kila mmiliki wa mashine ya kuzalisha unga ahakikishe unga unaozalishwa unaongezwa virutubisho.

Vilevile ameagiza kuanzishwa kwa Klabu za Lishe kwenye kila shule ambapo pamoja na shughuli nyingine shule kupitia klabu hizo zihakikishe zinakua na bustani za matunda na mbogamboga ili chakula wanachopata wanafunzi shuleni kiwe na mchanganyiko wenye virutubisho mbalimbali.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya ya Mbinga ametoa wito kwa wanaume kwenye jamii kushiriki utekelezaji wa afua za lishe kwa kushirikiana na wake zao badala ya jukumu hili muhimu la kutokomeza lishe duni na utapiamlo kuachiwa akimama na watoto pekee.

"Utekelezaji wa afua za lishe ni jukumu letu sote kuielimisha na kuihamasisha jamii kutambua umuhimu wa lishe  ili kukabiliana na udumavu, lakini wajibu wa lishe umebaki kwa wanawake na watoto tu, Ni wakati wetu sasa kuhakikisha jinsia ya kiume wanashiriki na kupata elimu ya lishe ili kuimarisha afya zetu" Amesisitiza DC Mangosongo.

Pia Mhe. Mangosongo ameagiza kuhuishwa kwa sheria ndogo za vijiji zinazowabana wazazi wenye watoto kushiriki utekelezaji wa afua za lishe pamoja na kuwapeleka kliniki kwa ajili chanjo, kufanya ufuatiliaji wa karibu na kutoa elimu pamoja na kuchukua hatua dhidi ya watoto wanaozaliwa na uzito pungufu pamoja na utapiamlo mkali

Imeandikwa na Salum Said 

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini 

9 Februari 2024

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit