Watumishi wa Serikali Wilaya ya Mbinga wametakiwa kujiridhisha na taarifa za taasisi zinazotoa mikopo kabla ya kuchukua mikopo kutoka katika taasisi husika.
Wito huo umetolewa tarehe 5 Machi 2024 na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mhe. Aziza Mangosongo katika kikao kazi kilichohusisha walimu, watendaji wa Kata pamoja na taasisi za mikopo zilizopo Wilayani Mbinga.
Mangosongo ameeleza kuwa kumekuwa na migogoro kati ya taasisi za mikopo pamoja na watumishi ambao ndio wakopaji adha ambayo inaathiri utendaji kazi wa watumishi hao.
Amefafanua kuwa moja ya sababu ya migogoro hiyo ni watumishi kuchukua mikopo kiholela bila kuwa na taarifa sahihi za taasisi hizo na kupelekea baadhi yao kutapeliwa fedha zao au kukatwa makato makubwa tofauti na makubaliano.
"Kuna taasisi za magumashi unaenda pale anakusainisha mkataba hakupi na akikupa mkataba wa kimagumashi na wewe una haraka ya hela mkataba husomi matokeo yake unatapeliwa" Amesema Mangosongo
Sambamba na hilo amewataka watumishi hao kujikita katika shughuli za kiuchumi na sio kutegemea mshahara pekee hali inayopelekea kujiingiza katika mikopo na kushindwa kulipa.
wakati huo huo amezitaka taasisi zote za zinazotoa mikopo Wilayani Mbinga kuhakikisha zina leseni ya biashara pamoja na kutoa mikopo kwa kuzingatia vigezo na miongozo.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Andrew Mbunda amebainisha kuwa kikao kazi hiko kinakwenda kuleta matokeo chanya na kubadilisha fikra za watumishi hao.
Akichangia mada katika kikao hiko mwalimu mstaafu Bw. Mtanga Mtanga amesema kuwa changamoto kubwa wanayokutana nayo ni riba kubwa za mikopo na kuacha kadi zao za benki jambo ambalo linalohatarisha usalama wa fedha zao.
Imeandikwa na Silvia Ernest
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
5 Machi 2024
MBINGA DISTRICT COUNCIL
Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA
Namba za simu: 2552640005
SImu ya mkononi: PS 0754533018
parua pepe: ded@mbingadc.go.tz
Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit