• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

KWAHERI MUTALEMWA, SANGA...KARIBU MARWA MBINGA DC

Tarehe ya kuwekwa: July 19th, 2021

Aliyekua Mweka Hazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Bw. Deodatus Mutalemwa pamoja na aliyekua Afisa Mapato wa Halmashauri hiyo, Bw. Elias Sanga wameagwa rasmi leo Julai 19 baada ya kupata uhamisho, katika hafla fupi iliyofanyika kwenye viwanja vya ofisi za Halmashauri vilivyopo Kiamili.

Hafla hiyo iliyoongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Ndg. Juma Mnwele na kuhudhuriwa na viongozi na watumishi wa Halmashauri hiyo waliopo Makao Makuu ya Halmashauri, Kiamili na Mkako imefanyika kufuatia watumishi hao kupata barua za kuhamishwa vituo vya kazi ambapo Bw. Mutalemwa anahamia Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma, huku Bw. Sanga akihamia Halmashauri ya Wilaya ya Songea, ndani ya Mkoa wa Ruvuma.

Kupitia Hafla hiyo, pia viongozi hao wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga wamemkaribisha mtumishi Samwel Marwa ambaye amehamia Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga akitokea Wilaya ya Tarime, Mkoa wa Mara ambapo anakuchukua nafasi ya Bw. Mutalemwa kama Kaimu Mweka Hazina.

Akizungumza kwa niaba ya watumishi, Mkurugenzi Mtendaji, Juma Mnwele amewashukuru watumishi hao waliohama kwa utumishi na utendaji wao kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga uliochangia kwa kiasi kikubwa kutengeneza sura njema ya Halmashauri na kwamba yeye binafsi na watumishi wengine wamejifunza mambo mengi kutoka kwao ikiwemo uvumilivu, jitihada, utashi na kujituma kwao kulikochangia kufanikisha mipango mingi ya Halmashauri na kuendana na sera ya serikali.

“Compliances za sera na sheria zote sisi tumezifanya karibu asilimia 100; hili jambo lingekua gumu sana kama DT asingekua na utashi” Amesema Mkurugenzi Mnwele akifafanua zaidi kuwa kwa kipindi cha miaka mitatu Halmashauri imeweza kupeleka fedha zote za miradi, kutoa fedha za mikopo ya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu sambamba na kulipa posho za madiwani.

Vilevile kwa niaba ya watumishi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Bw. Mnwele amemkaribisha Bw. Samwel Marwa ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga na kumhakikishia ushirikiano mkubwa kutoka kwake yeye binafsi, lakini pia kutoka kwa watumishi wote wa Halmashauri hiyo, huku akimpa wito wa kuendeleza na kuimarisha jitihada zaidi za ukusanyaji wa mapato.

“Tumefanya mambo mengi na mabadiliko mengi kwenye geti la Kitai kwa miaka hii mitatu, kwa sababu eneo lile karibu theluthi moja ya mapato yetu tunategemea pale ningekuomba sana utumie maarifa, muda wako na rasilimali tulizonazo kuona namna tutakavyoweza kupata suluhu ya eneo lile; kidogo bado tuna changamoto”. Amesisitiza Mkurugenzi Mnwele.

Imeandikwa na

Salum Said,

Afisa Habari, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

Tarehe 19, 2021 Kiamili


Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit