• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

MADIWANI MBINGA WAOMBA KUANGALIWA UPYA SOKO LA MAHINDI NFRA

Tarehe ya kuwekwa: August 31st, 2021

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Mkoani Ruvuma wameiomba serikali kuweka mfumo rafiki utakaowezesha soko la mahindi lililopo kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula, NFRA linawafikia na kuwanufaisha wakulima wadogo, badala ya mfumo uliopo sasa ambao unawanufaisha zaidi wafanya biashara, madalali na wakulima wakubwa.

Kupitia azimio lililowasilishwa wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani robo ya nne kwa mwaka wa fedha 2020/2021 kilichofanyika leo Agosti 31 katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Kigonsera, Madiwani hao pamoja na kuipongeza serikali kufuatia uamuzi wake wa kununua mahindi kupitia NFRA, lakini pia wameeleza kutoridhishwa kwao na mfumo uliopo na mwenendo mzima wa ununuzi wa zao hilo la mahindi.

Akiwasilisha azimio hilo kwa niaba ya madiwani, Mhe. William Mbwambo ambaye ni Diwani wa Kata ya Matiri na Katibu wa Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, amesema wao kama madiwani na wawakilishi wa wananchi wanaiomba serikali kutathmini hali ya mwenendo wa soko na kuona umuhimu wa kuboresha mfumo uliopo wa ununuzi wa zao la mahindi ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya vituo vya ununuzi na kiasi cha tani zitakazonunuliwa kupitia NFRA.

Mhe. Mbwambo amesema kwa kuzingatia hali ya uzalishaji na jiografia ya Wilaya ya Mbinga kituo pekee kilichopo cha Kigonsera hakimsaidii kabisa mkulima mdogo kwani Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ina takribani Kata nane zenye uzalishaji mkubwa wa zao la mahindi ambazo ni Mkako, Kigonsera, Amanimakolo, Namswea, Muungano, Matiri, Lukarasi na Ruanda lakini ni Kata ya Kigonsera tu ndio yenye kituo cha ununuzi wa zao hilo chini ya NFRA na ambacho kimepangiwa kununua tani 200 pekee za mahindi.

Aidha, ameongeza kuwa wakulima wengi wanashindwa kufikia soko hilo kutokana na umbali na gharama kubwa za usafirishaji kutoka kwenye maeneo ya uzalishaji hadi eneo kilipo kituo cha ununuzi, lakini pia hakuna utaratibu rasmi wa kuwatambua wakulima wadogo hali inayopelekea wakulima wengi kushindwa kuuza mahindi yao kupitia soko hilo na badala yake wameendelea kuuza mazao yao kwa bei ya chini ya wastani wa shilingi 12,000/= hadi 15,000/= kwa gunia kwenye maeneo waliyopo.

“Gharama ya kusafirisha gunia moja la mahindi kutoka kijiji cha barabara kata ya Matiri hadi Kigonsera ni shilingi 10,000, tunaiomba serikali ione uwezekano wa kusogeza vituo vya ununuzi kwenye maeneo yote yenye uzalishaji mkubwa ikiwa ni pamoja na kuainisha kiwango cha mahindi kitakachonunuliwa kutoka kwenye maeneo hayo ili kutoa fursa ya kuwafikia wakulima wengi zaidi kutoka kila eneo la uzalishaji”. Amesema Mhe. Mbwambo

Akifafanua kuhusu athari zinazoweza kujitokeza kutokana na wakulima wa zao la mahindi kuendelea kukosa soko la uhakika, Diwani Mbwambo amesema wakulima wengi watashindwa kumudu gharama kubwa za pembejeo kwa msimu ujao wa kilimo hali inayoweza kupelekea kushuka kwa uzalishaji, kuathirika kiuchumi na hatari ya kuzuka kwa baa la njaa.

Imeandikwa na

Salum Said

Afisa Habari, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga 

Agosti 31, 2021



Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit