• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

UWANJA WA KWANZA WA KISASA WA BASKETBALL WILAYANI MBINGA WAZINDULIWA

Tarehe ya kuwekwa: April 30th, 2021

Uwanja wa kwanza wa kisasa wa mpira wa kikapu (Basketball) Wilayani Mbinga umezinduliwa leo Aprili 30.

Hafla ya uzinduzi wa uwanja huo uliopo Shule ya Sekondari ya Wasichana Mbinga (Mbinga Girls) imefanyika shuleni hapo huku Mgeni Rasmi akiwa ni Afisa Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Bi. Amina Kibunde aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji ambaye pia aliambatana Afisa Elimu Sekondari, Mhandisi wa Ujenzi, Afisa Taaluma, Afisa Michezo na Afisa Utamaduni wa Halmashauri hiyo.

Bi. Amina ameongeza kusema kuwa michezo mashuleni imekua na umuhimu mkubwa katika kukuza afya ya mwili na akili na kutoa wito kwa viongozi na wanafunzi wa shule hiyo kutumia vema fursa ya uwepo wa uwanja huo shuleni hapo kwa kuhakikisha wanashiriki michezo kikamilifu huku wazingatia kutunza uwanja huo ili uweze kudumu kwa muda mrefu.

Naye Bi. Rehema Rohomoja ambaye ni Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Mbinga amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji na uongozi mzima wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwa kuwajengea uwanja huo wa kisasa huku akiahidi matumizi sahihi na matunzo ya uwanja huo na kwamba kutokana na umuhimu wa michezo katika kuboresha afya ya mwili na akili wanatarajia kuongeza kiwango cha ufaulu shuleni hapo

Awali akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa uwanja huo, Afisa Michezo Bw. Charles Maero amesema mradi huo umetekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga na kugharimu shilingi milioni 7, fedha zote zikiwa ni mapato ya ndani (Own Source)

Hafla ya uzinduzi wa uwanja huu imehudhuriwa pia na walimu na wanafunzi kutoka shule za sekondari za Mbinga Girls, Kigonsera, Kiamili, Mkako na Maposeni ambao pia wamepata fursa ya kushiriki midahalo na michezo mbalimbali.

Ujenzi wa uwanja huu ambao ni wa kwanza wa kisasa Wilayani Mbinga ni utekelezaji wa mkakati wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga katika kuboresha sekta ya michezo mashuleni.

Katika hatua nyingine Halmashauri imeendelea na uboreshaji wa uwanja wa michezo wa Shule ya Msingi Juhudi huku ikijiandaa kuanza ujenzi wa viwanja viwili kimoja kikiwa kwa ajili ya mpira wa miguu na kingine mpira wa kikapu Shule ya Sekondari ya Wavulana Mbinga (Mbinga Boys) iliyopo Ndongosi.

Imeandikwa na

Salum Said,

Afisa Habari, Mbinga D.C

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit