• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

MAAFISA UGANI NA WATENDAJI KATA WAPEWA PIKIPIKI MBINGA

Tarehe ya kuwekwa: April 19th, 2021

Watumishi 12 wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga wamezeshwa pikipiki ikiwa ni jitihada za Halmashauri hiyo katika kutatua changamoto ya usafiri na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Cosmas Nshenye ambaye alikua Mgeni Rasmi kwenye hafla ya ugawaji wa pikipiki hizo iliyofanyika Aprili 19, 2021 Shule ya Sekondari Kigonsera amempongeza Mkurugenzi na uongozi wa Halmashauri kwa kununua pikipiki hizo na kuomba mpango huo kuwa endelevu ili watumishi wote waliokusudiwa waweze kupata uwezeshwaji huo huku akiwaasa walionufaika na mgao huo wa pikipiki kuzingatia matumizi sahihi na yaliyokusudiwa.

Akimkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Mbinga kukabidhi pikipiki hizo kwa walengwa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Juma Mnwele amesema pikipiki hizo zenye thamani ya shilingi milioni 28 zimenunuliwa ikiwa ni awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mpango mkakati wa Halmashauri hiyo katika kutatua na kuondoa tatizo la usafiri na kuimarisha utoaji huduma kwa wananchi na kuahidi uendelevu wa mpango huo wa kuwezesha watumishi.

Bw.Mnwele ametoa rai kwa wote walionufaika na awamu hii kwa kuwakumbusha kuwa pikipiki hizo ni mali ya serikali, hivyo wanapaswa kuzingatia matumizi sahihi na yaliyokusudiwa na kuwasisitiza kujiepusha na ulevi kila mara wanapoendesha vyombo hivyo vya moto.

“Kama tunavyofahamu pikipiki haina urafiki na mlevi, na kama ambavyo watu husema ukinywa bia moja na pikipiki nayo hunywa bia moja; vilevile unapokunywa bia nne pikipiki nayo inakunywa bia nne. Maana yangu ni kuwa msiendeshe pikipiki mkiwa mmelewa”. Amesisitiza Mkurugenzi huyo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Mhe. Desderius Haule amesema pikipiki hizo zimenunuliwa ikiwa ni utekelezaji wa maazimio ya vikao juu ya kutenga fedha na kuhakikisha wanatatua kero ya usafiri kwa watumishi wa Halmashauri hiyo na kuongeza kuwa hategemei matukio ya upotevu wala uharibifu wowote yatakayosababishwa na uzembe na wao kama madiwani watasimamia kikamilifu kwenye maeneo yao.

“Kwa kuwa ni fedha za Halmashauri tutakapoona aliyekabidhiwa hajali usalama wa chombo hatutasita kubadilisha matumizi; tunaweza tukanunua baiskeli tukakupa badala yake ambayo pengine ndio utakua na uwezo wa kuitunza. Sina maana kwamba mnyang’anywe, ninachosisitiza pikipiki hizi ziwe ni kwa ajili ya utendaji kazi na ziwasadie kuwahudumia wananchi”. Amesema mwenyekiti huo.


Orodha na mchanganuo wa  watumishi waliopata pikipiki kwenye awamu hii ya kwanza ni Maafisa Kilimo wa Kata 6 za Langiro, Linda, Amani Makolo, Mbuji, Namswea na Matiri, Watendaji wa Kata 4 za Matiri, Kigonsera, Kipapa na Muungano. Wengine ni Maafisa Mifugo wa Kata 2 za Mkumbi na Mikalanga.

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imekua na utaratibu wa mara kwa mara wa kuwezesha watumishi wake kwa namna na njia mbalimbali ikiwa ni utekelezaji wa sera na mpango wa Halmashauri hiyo ya kuwezesha watumishi wake. Ikumbukwe ndani ya mwaka huu wa fedha 2020/2021 mnano mwezi Disemba jumla ya walimu 105 walioajiriwa na kupangiwa kufanya kazi kwenye shule za msingi na sekondari ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga waliwezeshwa na Halmashauri hiyo kwa kupatiwa magodoro na majiko ya gesi yenye thamani ya shilingi milioni 27.3  

   

Imeandikwa na:

Salum Said

Afisa Habari

HALMASHAURI YA WILAYA YA MBINGA.  Aprili 17, 2021

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit