• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

MHE. BASHUNGWA ATOA RAI SERIKALI KUJITANGAZA KUPITIA MAAFISA HABARI

Tarehe ya kuwekwa: May 24th, 2021

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa amewaagiza Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini kujituma kwa kasi, ari na weledi katika utoaji taarifa na huduma za habari kwa umma juu ya masuala mbalimbali yanayotekelezwa na serikali ikiwemo miradi ya maendeleo.

Mhe.Bashungwa ameyasema hayo Mei 24, 2021 Jijini Mbeya wakati akifungua Kikao Kazi cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano wa Serikali katika Ukumbi wa Mikutano uliopo Chuo cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST), ambapo amesisitiza kuwa utoaji wa taarifa kwa umma ni takwa la kisheria na jamii ina haki ya kuhabarishwa huku akisema maafisa habari ndio watekelezaji wakubwa wa sheria hizo.

"Nimeguswa na Kauli Mbiu ya kikao hiki kwa mwaka huu isemayo Utoaji Taarifa kwa Umma ni Takwa la Kisheria Viongozi wa Umma na Maafisa Habari Tuwajibike, Hivyo Wizara ninayoisimamia inaendelea kufanya mageuzi makubwa katika kusimamia utoaji wa huduma za habari kwa umma, na hii ni utekelezaji wa Sheria ya Huduma ya Habari ya Mwaka 2016, na Sheria ya Haki ya Kupata Habari ya Mwaka 2016" amesisitiza Mhe. Bashungwa.

Aidha Mhe.Bashungwa ametumia nafasi hiyo kuwahakikishia Maafisa Habari kuwa Wizara yake inatambua changamoto mbalimbali zinazowakabili maafisa hao ikiwemo ukosefu na ufinyu wa bajeti, kukosa zana za kisasa na vitendea kazi muhimu kama camera, lens, computer, internet na mawasiliano, baadhi yao kutoshirikishwa kwenye vikao na ziara muhimu, pamoja na kukosa mafunzo ya mara kwa mara kulingana na mabadiliko ya teknolojia hali inayopelekea wengi wao kufanya kazi kwenye mazingira magumu.

Mhe. Waziri amewahahakishia maafisa habari hao kuwa serikali kupitia Wizara ya Habari kwa kushirikiana na Wizara nyingine hususani TAMISEMI imekusudia na kujipanga kushughulikia kikamilifu changamoto zote wanazokabiliana nazo huku akitoa wito kwa viongozi wa Wizara, Taasisi, Wakala na Mamlaka za Serkali za Mitaa kuhakisha wanatoa na kuwapa ushirikiano mzur maafisa habari hao ambao ndio washauri wakuu wa masuala ya habari kwenye maeneo yao.

Hata hivyo wakati kikao kinaendela Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Dkt. Abbasi alipokea ujumbe wa simu kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwenye kikao hicho ambapo akisoma ujumbe huo wa Mhe. Rais, Dkt.Abbasi amenukuu

"Naomba muendelee kuhimizana kuhusu umuhimu wa taarifa kwa Umma, yale yasiyo mazuri na yasiyo ya lazima kuwe na namna bora ya kutoa taarifa na msiache kusema mpaka wananchi waanze kulalamika ndiyo watoe taarifa"

Kikao Kazi hiki cha siku tano cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano wa Serikali kitakachofanyika Mei 24-28 kimehudhuriwa pia na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Dkt. Hassan Abbasi, Katibu Mkuu OR-TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe,  Naibu Katibu Mkuu Habari, Dkt. Ally Possi, Naibu Waziri wa Habari Mhe. Pauline Gekul, na viongozi wengine wa Wizara na Mkoa wa Mbeya wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Juma Homera.

Imeandikwa na

Salum Said

Afisa Habari, Mbinga D.C

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit