• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima

BENKI YA NMB YAWEZESHA PIKIPIKI KWA MAAFISA USHIRIKA MBINGA NA NYASA

Tarehe ya kuwekwa: December 30th, 2022

Leo Ijumaa Disemba 30, 2022 Benki ya NMB imekabidhi pikipiki 3 kwa maafisa Ushirika kutoka Halmashauri za Mkoa wa Ruvuma zinazolima Kahawa ili kuongeza tija katika usimamizi, ufuatiliaji na uzalishaji wa zao hilo.

Hafla ya makabidhiano ya Pikipiki hizo imefanyika Ijumaa kwenye Ofisi za NMB Mbinga Mjini ambapo Kaimu Meneja wa NMB Tawi la Mbinga Anold Mwakabage amekabidhi pikipiki 3, kadi za usajili, kofia ngumu, na viakisi mwanga (reflectors) kwa Maafisa Ushirika kutoka Halmashauri za Wilaya ya Mbinga, Mji wa Mbinga na Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa.

Akikabidhi pikipiki hizo Bw. Mwakabage amesema kufuatia kikao cha wadau wa zao la Kahawa kilichofanyika mwezi Mei mwaka huu 2022 wao kama Benki na wadau wakubwa wa zao hilo na kilimo kwa ujumla waliona kuna umuhimu wa kuwezesha vitendea kazi hasa usafiri kwenye Ofisi za Ushirika za Halmashauri hizo tatu ili kurahisisha ufuatiliaji na utoaji wa huduma za ugani kwa wakulima na vyama vya ushirika.

Aidha Afisa Uhusiano NMB Mbinga Joseph Raphael Rimoy amesema kwa kutambua umuhimu wa Ofisi za Ushirika kwenye Halmashauri na changamoto zilizopo za kijiografia kwenye maeneo ya vijijini wanakofanyia kazi wao kama Benki na wadau wametoa pikipiki hizo wakiamini zitasaidia kurahisisha wakulima wengi zaidi kufikiwa katika suala zima la upatikanaji wa huduma za ugani kutoka Ofisi za Ushirika.

"Sisi kama Benki ya NMB tukaona tutoe vitendea kazi hivi ili kuwezesha kuwafikia wakulima wengi zaidi na kwa muda mfupi ikizingatiwa jiografia ya maeneo yetu kulinganisha na rasilimali za usafiri zilizopo kwenye Halmashauri" Ameongeza Bw. Rimoy.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga mara baada ya kupokea pikipiki Afisa Ushirika Noel Ngailo ameishukuru Benki ya NMB kwa uwezeshwaji huo na kwamba wao kama watendaji wa sekta ya Kilimo na Ushirika kwenye Halmashauri wamejipanga kikamilifu kuwahudumia wakulima na vyama vya ushirika kwa urahisi, haraka na kwa ufanisi zaidi.

"Tunashukuru kwa ushirikiano huu uliopo baina ya sekta binafsi kupitia Benki ya NMB Tawi la Mbinga na Serikali kupitia Halmashauri zetu tatu na vitendea kazi hivi vitaturahisishia sana kuwatembelea wakulima, kuwasikiliza na kutatua kero zao kwa haraka zaidi " Amefafanua Bw. Ngailo

Imeandaliwa na 

Salum Said, Kitengo cha Mawasiliano Serikalini 

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga 

Tarehe 30 Disemba, 2022

Matangazo

  • MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 December 18, 2022
  • MAELEKEZO KWA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA SHULE ZA BWENI 2023 December 18, 2022
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI ENEO LA KIAMILI October 13, 2021
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MBINGA DC KUWA MFANO UTEKELEZAJI WA MRADI MKUBWA WA UMILIKISHAJI ARDHI NCHINI

    January 11, 2023
  • MBINGA DC YAKAMILISHA UJENZI WA MADARASA MAPYA 10

    January 06, 2023
  • BENKI YA NMB YAWEZESHA PIKIPIKI KWA MAAFISA USHIRIKA MBINGA NA NYASA

    December 30, 2022
  • KAMATI YA SIASA YATEMBELEA KITUO CHA AFYA MKUMBI

    December 29, 2022
  • Tazama zote/kote

Video

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mh. Christine Mndeme aagiza Halmashauri ya Wilaya kuhamiamia Kiamili kabla ya tarehe 30/10/2019
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Iringa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit