• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

BENKI YA NMB YAWEZESHA PIKIPIKI KWA MAAFISA USHIRIKA MBINGA NA NYASA

Tarehe ya kuwekwa: December 30th, 2022

Leo Ijumaa Disemba 30, 2022 Benki ya NMB imekabidhi pikipiki 3 kwa maafisa Ushirika kutoka Halmashauri za Mkoa wa Ruvuma zinazolima Kahawa ili kuongeza tija katika usimamizi, ufuatiliaji na uzalishaji wa zao hilo.

Hafla ya makabidhiano ya Pikipiki hizo imefanyika Ijumaa kwenye Ofisi za NMB Mbinga Mjini ambapo Kaimu Meneja wa NMB Tawi la Mbinga Anold Mwakabage amekabidhi pikipiki 3, kadi za usajili, kofia ngumu, na viakisi mwanga (reflectors) kwa Maafisa Ushirika kutoka Halmashauri za Wilaya ya Mbinga, Mji wa Mbinga na Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa.

Akikabidhi pikipiki hizo Bw. Mwakabage amesema kufuatia kikao cha wadau wa zao la Kahawa kilichofanyika mwezi Mei mwaka huu 2022 wao kama Benki na wadau wakubwa wa zao hilo na kilimo kwa ujumla waliona kuna umuhimu wa kuwezesha vitendea kazi hasa usafiri kwenye Ofisi za Ushirika za Halmashauri hizo tatu ili kurahisisha ufuatiliaji na utoaji wa huduma za ugani kwa wakulima na vyama vya ushirika.

Aidha Afisa Uhusiano NMB Mbinga Joseph Raphael Rimoy amesema kwa kutambua umuhimu wa Ofisi za Ushirika kwenye Halmashauri na changamoto zilizopo za kijiografia kwenye maeneo ya vijijini wanakofanyia kazi wao kama Benki na wadau wametoa pikipiki hizo wakiamini zitasaidia kurahisisha wakulima wengi zaidi kufikiwa katika suala zima la upatikanaji wa huduma za ugani kutoka Ofisi za Ushirika.

"Sisi kama Benki ya NMB tukaona tutoe vitendea kazi hivi ili kuwezesha kuwafikia wakulima wengi zaidi na kwa muda mfupi ikizingatiwa jiografia ya maeneo yetu kulinganisha na rasilimali za usafiri zilizopo kwenye Halmashauri" Ameongeza Bw. Rimoy.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga mara baada ya kupokea pikipiki Afisa Ushirika Noel Ngailo ameishukuru Benki ya NMB kwa uwezeshwaji huo na kwamba wao kama watendaji wa sekta ya Kilimo na Ushirika kwenye Halmashauri wamejipanga kikamilifu kuwahudumia wakulima na vyama vya ushirika kwa urahisi, haraka na kwa ufanisi zaidi.

"Tunashukuru kwa ushirikiano huu uliopo baina ya sekta binafsi kupitia Benki ya NMB Tawi la Mbinga na Serikali kupitia Halmashauri zetu tatu na vitendea kazi hivi vitaturahisishia sana kuwatembelea wakulima, kuwasikiliza na kutatua kero zao kwa haraka zaidi " Amefafanua Bw. Ngailo

Imeandaliwa na 

Salum Said, Kitengo cha Mawasiliano Serikalini 

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga 

Tarehe 30 Disemba, 2022

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit