Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

CCM MBINGA WAHITIMISHA SHEREHE ZA WIKI YA WAZAZI KWA KUFANYA USAFI HOSPITALI YA HALMASHAURI

Tarehe ya kuwekwa: April 18th, 2024

Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mbinga tarehe 18, 2024 imeshiriki zoezi la usafi na utunzaji wa mazingira katika  Hospitali mpya ya Halmashauri iliyopo Kigonsera Wilayani Mbinga Mkoa wa Ruvuma.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mbinga Ndg. Hajiri Methew Kapinga amewaongoza wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya hiyo kufyeka nyasi na kupanda miti kwenye maeneo yanayozunguka hospitali ya Halmashauri ikiwa ni katika kuhitimisha Sherehe za Wiki ya Wazazi kiwilaya zilizofanyika Kata ya kigonsera, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga.

Sambamba na kushiriki zoezi hilo la usafi na utunzaji wa mazingira, Jumuiya hiyo imetembelea miundombinu ya hospitali ambayo ujenzi wake umekamilika lakini pia imekagua maendeleo ya miundombinu mipya ambayo ujenzi wake bado unaendelea.

Akizungumza mara baada ya zoezi hilo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Ndg. Hajiri Kapinga ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwa kusimamia vizuri mradi huo wa Hospitali ya Halmashauri huku akiipongeza Serikali ya chama cha mapinduzi kwa kuwasogezea karibu wananchi huduma hiyo muhimu na hivyo kusaidia kuokoa maisha ya wananchi wa Mbinga na watanzania kwa ujumla.

Naye Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mbinga Ndg. Angelo Madundo amesema wao kama Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya hiyo wanampongeza na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa usimamizi mzuri wa Ilani ya Uchaguzi.

 "Sisi kama Jumuiya ya Wazazi Mbinga tunaungana na wazazi wote kumpongeza Rais wetu na Mwenyekiti wa CCM Taifa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya ya kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 ikiwemo ujenzi wa hospitali hii ya wilaya ya Mbinga iliyojengwa kwa viwango ambayo mpaka sasa ujenzi wake umegharimu zaidi ya shilingi Bilioni 2.3" Amesema Ngd. Madundo.

Imeandikwa na Salum Said,

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali

Tarehe 18 Aprili, 2024

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit