• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

DC MBINGA APATA 'MWAROBAINI' UHABA MBOLEA YA RUZUKU

Tarehe ya kuwekwa: December 6th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mhe. Aziza Mangosongo leo Jumanne Disemba 6, 2022 amekutana na kufanya mazungumzo na wadau wa kilimo kujadili hali ya upatikanaji wa pembejeo za kilimo wilayani Mbinga.

Kikao hicho kilichofanyika katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya kimekutanisha viongozi mbalimbali wa Wilaya na Halmashauri, Maafisa Kilimo na Ushirika, wauzaji na maawakala wa pembejeo za kilimo pamoja na viongozi kutoka Chama Kikuu cha Ushirika Mbinga (MBIFACU) na Vyama vya Msingi vya Ushirika (AMCOS) kutoka maeneo yote ya Wilaya ya Mbinga.

Kikao hicho kimefanyika ili kujadiliana na kupata muafaka na makubaliano ya pamoja kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazopelekea upatikanaji hafifu wa pembejeo za kilimo hususani mbolea ya ruzuku miongoni mwa wakulima wa Wilaya ya Mbinga katika kipindi hiki ambacho tayari msimu wa kilimo ukiwa tayari umeanza.

Akifungua kikao Mkuu wa Wilaya alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuipa kipaumbele sekta ya kilimo baada ya kuongeza bajeti ya Wizara na kuweka utaratibu mzuri wa ruzuku kwenye pembejeo na kwamba kupitia utaratibu huo uliowekwa na Serikali ya Awamu ya Sita uzalishaji wa mazao ya kilimo na mnyororo wa thamani kwenye mazao ya kilimo unatarajiwa kuongezeka kwa kiwango kikubwa msimu ujao wa mavuno

Kwa mujibu wa tarifa ya mapokezi ya mbolea msimu huu wa 2022/2023 iliyowasilishwa mbele ya Mkuu wa Wilaya na Maafisa Kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga na Halmashauri ya Mji wa Mbonga imeelezwa hadi jana Disemba 6 kiasi cha tani 5,061 pekee za mbolea ndizo zimepokelewa na kuuzwa kwa wakulima kwenye Halmashauri zote mbili kati ya tani 18,861 zinazohitajika sawa na asilimia 26.8% huku changamoto zikielezwa kuwa ni pamoja na uhaba wa mawakala na vituo vya kuuzia mbolea pamoja na kile kilichoelezwa kuwa hata mawakala wachache waliopo hawana mbolea ya kutosha kuweza kukidhi mahitaji ya wakulima.

Aidha kupitia kikao hicho DC Mangosongo ameunda Kamati maalum itakayokua na jukumu la kufuatilia, kutatua na kuziwasilisha moja kwa moja Wizara ya Kilimo changamoto zote zilizobainishwa kuchangia kuzorotesha hali ya upatikanaji wa mbolea ya ruzuku huku akitoa wito kwa Chama Kikuu MBIFACU kuzisimamia AMCOS zote na kuhakikisha zinawasaidia wanachama wake na wakulima waliopo kwenye maeneo yao ambayo hakuna mawakala wanapata mbolea kwa wakati.

Imeandikwa na 

Salum Said 

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini 

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga 

6 Disemba, 2022

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit