• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

DC MBINGA ATOA WITO WANANCHI KUCHANGAMKIA CHANJO UVIKO-19

Tarehe ya kuwekwa: August 6th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Mhe. Aziza Mangosongo ametoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa ya kupata chanjo ya UVIKO-19 inayotolewa bure nchini ili kukabiliana na maambukizi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Corona (Covid-19).

Mhe. Mangosongo ametoa wito huo leo Agosti 6 wakati alipoongoza zoezi la uzinduzi rasmi wa utoaji wa chanjo ya ugonjwa wa virusi vya Corona (Uviko 19), tukio lililofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Oddo Mwisho uliopo Ofisi za Halmashauri ya Mji wa Mbinga Mkoani Ruvuma.

Akizungumza na viongozi wa Taasisi mbalimbali za Umma na binafsi, viongozi wa dini, makampuni na wadau wengine waliohudhuria hafla hiyo ya uzinduzi wa chanjo ya UVIKO-19, DC Mangosongo amesema tukio hilo ni sehemu ya kupeana taarifa za ziada kuhusu hali ya maambukizi ya Ugonjwa unaosababishwa na Virusi vya Corona nchini pamoja na kuendelea kukumbushana kuhusu hatua muhimu za kuchukua ili kuendelea kukabiliana na wimbi la tatu la UVIKO-19 Wilayani Mbinga

Mhe. Mangosongo amesema kulingana na hali ya maambukizi ya UVIKO-19 duniani na mwenendo wa ugonjwa huo nchini na katika nchi jirani ni wazi kuwa Wilaya yetu ya Mbinga, Mkoa wa Ruvuma na Taifa kwa ujumla hatupo salama na hivyo jitihada za makusudi zinahitajika ili kukabiliana na wimbi la kuenea kwa virusi hatari vya Corona na kwamba kupata chanjo ya UVIKO-19 ni hatua mojawapo na muhimu katika kukabiliana na virusi hivyo hatari..

“…hatuwezi kusema tuko salama, hivyo ni lazima juhudi za makusudi za kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huu katika Wilaya yetu ya Mbinga zichukuliwe kwa uzito unaostahili, ila iwe kwa kuleta uelewa sahihi bila kuwatisha na kuwaogopesha wananchi”. Amesema Mkuu huyo wa Wilaya.

Aidha Mhe. Mangosongo ametoa maelekezo kwa viongozi wa ngazi zote kuonesha mfano kwa wananchi kwa kuchukua hatua zote za tahadhari za kujikinga dhidi ya UVIKO-19 huku akiagiza taasisi na maeneo yote ya kutolea huduma kuweka utaratibu wa kupunguza misongamano kwenye maeneo hayo bila kuathiri shughuli za kiuchumi na kitaasisi, kusimamia upatikanaji wa vifaa kinga kama Barakoa, Maji tiririka na Sabuni, Vipukusi mikono (Sanitizer), vipima joto (Thermal scanners) na kuhakikisha vifaa hivyo vinatumika kikamilifu wakati wote.

Amesema “Halmashauri zihakikishe maeneo yote ya umma kama vile stendi za mabasi na malori, vituo vya Bajaji na Bodaboda, bustani za kupumzika, Masoko, Misikiti, Makanisa na sehemu za burudani zinakuwa na vifaa vya kunawia mikono, maji safi tiririka na sabuni na kuhakikisha vinatumika”

Ametoa wito kwa viongozi wa dini kuhakikisha waumini wote wanachukua tahadhari zote za kujikinga na UVIKO-19 wakati wa ibada ikiwemo kuvaa barakoa, kukaa umbali usiopungua mita moja baina ya mtu na mtu sambamba na kufupisha muda wa ibada huku akisitisha mikusanyiko yote Wilayani Mbinga hadi hapo ugonjwa utakapodhibitiwa.

“Nasitisha mikusanyiko yote mikubwa ya kijamii, kidini na kisiasa mpaka ugonjwa utakapodhibitiwa na kutolewa taarifa rasmi na Wizara ya Afya; Aidha, kwa mikusanyiko ya lazima wananchi watalazimika kuomba kibali kutoka kwenye mamlaka husika” Amesema DC Mangosongo.

Naye Mganga Mkuu, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Dkt. Louis Chomboko amebainisha vituo vitakavyotoa huduma ya chanjo ya UVIKO-19 kwa Halmashauri hiyo kuwa ni Zahanati ya Mkako, Kituo cha Afya Mapera na Hospitali ya Misheni Litembo kuanzia Jumatatu Agosti 9 na kwamba kipaumbele kitatolewa kwa watumishi wa sekta ya afya, watu wenye umri wa zaidi ya miaka 50 na wale wenye magonjwa sugu.

Imeandikwa na 

Salum Said,

Afisa Habari, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

Agosti 6, 2021


Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit