• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

D.C MBINGA AWATAKA WATU WENYE ULEMAVU KUACHA “KUJINYANYAPAA”

Tarehe ya kuwekwa: April 16th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mhe. Cosmas Nshenye amewataka watu wenye ulemavu kuchangamkia fursa ya mikopo inayotolewa na serikali kwa kuhakikisha wanarejesha fedha wanazokopa kwa wakati na kuiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kusimamia suala hilo kikamilifu ili fedha hizo ziweze kunufaisha watu wengine.

Mhe. Nshenye amesema hayo wakati wa kikao cha kutathmini changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu Wilayani Mbinga kilichofanyika leo Aprili 16 katika Ukumbi wa Safina uliopo Kigonsera, huku pia akiwataka watu hao kujiamini na kukubaliana na hali ya ulemavu waliyonayo kwa kusema watu wenye ulemavu wana haki zote na wajibu kama watu wengine.

Akizungumza kwenye kikao hicho, Mhe. Mkuu wa Wilaya amesema watu wenye ulemavu wanapaswa kujiona wenye bahati kwani serikali imewajali kwa kuwatengea asilimia maalumu ya fedha za mikopo licha ya watu hao kuwa na sifa nyingine za ziada za kupatiwa mikopo hiyo kupitia makundi ya vijana na wanawake.

Sambamba na hilo, pia Mhe. Nshenye ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kuhakikisha suala la urejeshwaji wa fedha za mikopo linasimamiwa kikamilifu na kwa mujibu wa sheria na kuwaasa watu wenye ulemavu kuacha kulalamika na kufuta mawazo ya kujinyanyapaa huku akiwataka watu hao kuwa na fikra za kijasiriamali na kujipanga kurejesha fedha za mikopo kama inavyofanywa na wajasiriamali wengine wanaonufaika na mikopo ya 10% ya fedha za mapato ya ndani zinazotengwa na kutolewa na Halmashauri hiyo.

“Watu wa Halmashauri ukifika muda sheria hizi zitumike bila ubaguzi, hawa wote ni wajasiriamali na fedha hizi ni za watu wote..,hatuwezi kuwa na na vikundi visivyorejesha mikopo yao”. Ameongeza Mkuu huyo wa Wilaya.

Bw. Paschal Ndunguru, ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga amesema Halmashauri hiyo imekua ikitoaji mikopo ya wajasiriamali kwa vikundi vya watu wenye ulemavu kama sehemu ya jitihada zake za kuwezesha watu wenye ulemavu lakini vikundi hivyo vimekuwa na mwitikio hafifu wa kurejesha fedha hizo jambo linalopelekea kushindwa kuwezesha vikundi vingine vingi zaidi na kwa wakati.

Bw. Paschal amefafanua kuwa kwa miaka mitatu mfululizo kuanzia 2018/2019 hadi mwaka huu 2020/2021 Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imewezesha fedha jumla ya shilingi Milioni 98 kwa vikundi vya watu wenye ulemavu lakini fedha ambazo zimerejeshwa hadi sasa ni Milioni 30.6 pekee.

Awali wakizungumza mbele ya Mkuu wa Wilaya, viongozi wa Chama cha Watu Wenye Ulemavu (CHAWATA) na Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemamavu (SHIVYAWATA) Wilayani Mbinga wameshukuru kwa uwezeshwaji wa fedha ambao umekua ukifanywa na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga lakini pia wanaomba serikali kuendelea kuwajengea uwezo kwa kuwapa elimu ya ujasiriamali.

Pia viongozi hao wameiomba serikali kuona uwezekano wa kuweka ruzuku kwenye nyenzo na vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu ikiwa ni pamoja na kuweka watoa huduma ambao ni wakalimani wa lugha za alama kwenye maeneo ya kutolea huduma kama hospitali, mahakama, na vituo vya polisi.

Imeandikwa na:

Salum Said

Afisa Habari

HALMASHAURI YA WILAYA YA MBINGA.  Aprili 16, 2021

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit