• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

DED MNWELE AONGOZA HARAMBEE KUCHANGIA UJENZI KANISA LA KIAMILI

Tarehe ya kuwekwa: June 27th, 2021

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Juma Mnwele leo Juni 27, 2021 ameshiriki ibada ya misa takatifu na kuongoza harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa la Kigango cha Kiamili, Parokia ya Kigonsera Jimbo la Mbinga.

Ibada hiyo imefanyika kwenye viwanja vya Kigango cha Kiamili na kuongozwa na Padre Silverius Mwingira ambaye amemwakilisha Paroko wa Parokia ya Kigonsera, Paroko Thadeo Kinyero.

Akizungumza kwenye Harambee hiyo ya kuchangia ujenzi wa Kanisa Mkurugenzi Mnwele, ambaye alikua Mgeni Rasmi kwenye hafla hiyo ametoa wito kwa jamii hasa waumini kuchangia kwa moyo wote na kujitolea nguvu kazi ili kuharakisha ujenzi wa kanisa hilo na kuhakikisha wanaweka suala la kuchangia ujenzi kama ajenda ya kudumu kila wanapokutana kupitia Jumuiya zao.

Aidha Bw. Mnwele amesema anatambua kuwa kukamilika kwa kanisa hilo kutarahisisha utoaji wa huduma za kiroho kwa jamii ya eneo zima la Kiamili wakiwemo watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ambao wanaoishi na kufanya kazi makao makuu ya Halmashauri yaliyopo hapo Kiamili.

Bw. Mnwele ameongeza kuwa Kanisa hilo pia litakua tegemeo kubwa kwa wanafunzi na watumishi wa Shule za Sekondari za Kiamili, Kampala, Shule ya Sekondari ya Wasichana Mbinga (Mbinga Girls) na Shule ya Msingi Juhudi ambazo zote zipo eneo hilo la Kiamili

Akiongoza harambee hiyo Mkurugenzi Mnwele amechangia fedha tasilimu shilingi Laki Tano (Tshs.500,000/=) kama mchango wake binafsi huku akiahidi Ofisi yake kuchangia mifuko 200 ya saruji pamoja na bati 100 aina ya IT-5 (Msauzi).

Katika Harambee hiyo jumla ya fedha tasilimu shilingi 4,285,400 zimepatikana, huku ahadi zilizotolewa zikiwa ni fedha zaidi ya shilingi Laki Saba, mifuko 215 ya Saruji na bati 200.

Awali katika mahubiri yake, Padre Mwingira alisisitiza juu ya kumuamini na kumtegemea mungu katika maisha yetu ya kila siku na umuhimu wa jamii kujitoa na kumtolea mungu katika kulijenga kanisa.

Aidha Padre huyo ametoa wito kwa jamii kujitolea na kushiriki ujenzi na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na serikali akitolea mfano miradi ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya na Ofisi za Halmashauri inayojengwa hapo Kiamili

Imeandikwa na

Salum Said, Afisa Habari Mbinga D.C

Juni 27, 2021



Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit