• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

ELIMU BORA YA UNYONYESHAJI MSINGI WA LISHE BORA

Tarehe ya kuwekwa: November 9th, 2021

Elimu ya unyonyeshaji imetakiwa kuwekewa mkazo na kupewa kipaumbele ikiwa ni katika jitihada za kukabiliana na hali duni ya lishe na utapiamlo mkali kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

Hayo yamejiri wakati wa kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mikataba ya lishe kilichofanyika leo Novemba 9, 2021 Kiamili Wilayani Mbinga kujadili namna wataalam wa afya na watendaji katika ngazi mbalimbali wanavyoshiriki mapambano dhidi ya utapiamlo na kuhakikisha jamii inaendelea kuwa na lishe bora Wilayani humo.

Katika kikao hicho kilichoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Mhe. Aziza Mangosongo, na kuhudhuriwa na wataalam na Maafisa Watendaji wa Kata zote 29 za Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imeelezwa kuwa unyonyeshaji wa watoto usiozingatia maelekezo ya wataalam unaofanywa na sehemu kubwa ya akinamama mara baada ya kujifungua ni moja ya sababu zinazochangia kuwa na hali duni ya lishe na hata kupelekea baadhi ya watoto kupata utapiamlo mkali.

Akizungumza kwenye kikao hicho Mhe. Aziza ametoa rai kwa wataalam kuweka mkazo zaidi katika kutoa elimu ya namna bora ya unyonyeshaji kwa jamii huku akikemea vikali kile kilichoelezwa tabia ya baadhi ya wanaume kunyonya maziwa ya waenza wao wanaonyonyesha na hivyo kuwakosesha watoto virutubisho muhimu, hali inayoweza kupelekea watoto kuwa na hali duni ya lishe.

Kufuatiwa kikao hicho watendaji wa Kata za Kitura, Kigonsera na Nyoni wamepongezwa kwa kufanya vizuri katika kusimamia suala la lishe kwa kipindi cha Julai hadi Septemba 2021, huku Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Mhe. Desderius Haule akipongeza utaratibu uliowekwa na Halmashauri hiyo wa kushindanisha kata na kuwatunuku zawadi Watendaji wa Kata zinazofanya vizuri.

“Kama hawa wamefanya vizuri na kushinda leo, kikao kijacho tuone kata nyingi zimefanya vizuri zaidi”. Ameongeza Mhe. Haule na kuhitimisha kuwa lishe ni suala la kimkakati kitaifa, na kwamba usimamizi thabiti wa afua za lishe kuanzia ngazi za chini (Vijiji na Kata) kutapelekea Wilaya, Mkoa na Taifa kwa ujumla kufanya vizuri na kuwa na jamii yenye lishe bora, kuongeza uzalishaji na kukuza uchumi wa nchi.

Kikao hicho kimefuatiwa na utiaji saini na uhuishwaji wa mikataba ya lishe ngazi ya Wilaya, Kata na Vijiji ambapo Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji, Katibu Tawala na Mganga Mkuu wa Wilaya wametia saini kwa ngazi ya Wilaya Huku Maafisa Watendaji Kata wakitia saini mikataba hiyo kwa upande wa Kata na Vijiji.

Imeandikwa na

Salum Said, 

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga 

Tarehe 9 Novemba, 2021

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • WATAALAM OR-TAMISEMI WARIDHISHWA NA MIRADI YA MBINGA DC

    July 17, 2025
  • SHILINGI 1,544,770,750.00 ZATUMIKA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA AFYA

    July 15, 2025
  • KIKAO CHA TAHMINI UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA 2024/2025

    July 15, 2025
  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit