• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

HALMASHAURI YAMUWEZESHA VIFAA SAIDIZI MTOTO BARAKA MWENYE ULEMAVU WA VIUNGO

Tarehe ya kuwekwa: January 18th, 2024

Mtoto Baraka Nicolaus Mbunda mwenye umri wa miaka 12 na mwenye mahitaji maalum kutokana na ulemavu wa viungo alionao baada ya kuzaliwa bila miguu na mikono, hatimaye amewezeshwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwa kupatiwa vifaa saidizi.

Baraka ambaye ni mwanafunzi wa darasa la pili shule ya msingi Huruma amekabidhiwa vifaa hivyo Januari 16, 2024 na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mhe. Desderius Haule wakati alipomtembelea shuleni hapo kujionea hali halisi ya changamoto zinazomkabili.

Mwenyekiti Haule amemkabidhi mtoto Baraka vifaa ambavyo ni kiti-mwendo au kiti cha magurudumu (wheelchair) pamoja na kiti maalum kinachosaidia mtu mwenye mahitaji maalum wakati wa kupata haja kubwa na ndogo ikiwa ni hatua za awali zilizochukuliwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga katika kumpunguzia adha na changamoto mtoto huyo kutokana na hali ya ulemavu aliyonayo.

Mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo Mhe. Haule amebainisha kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga itaendelea kufuatilia kwa ukaribu maendeleo ya mtoto Baraka na kwamba kuna jitihada mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa katika kuwafikia watoto wengi zaidi wenye mahitaji maalum na kushughulikia changamoto zinazowakabili ikiwemo ujenzi wa shule maalum ya watu wenye ulemavu inayojengwa Kata ya Maguu.

“Halmashauri itafanya kila kitakachowezekana kuhakikisha mtoto Baraka anasoma na kufikia ndoto zake kama alivyoeleza mwenyewe hapa kwamba anataka asome hadi awe Daktari” Amesisitiza Mwenyekiti Haule.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo wa Halmashauri ametoa wito kwa wazazi na walezi pamoja na jamii kwa ujumla kutowaficha watoto wenye ulemavu na kwamba wanatakiwa kuthaminiwa na kupewa haki kama watoto wengine.

Akizungumzia hali ya taaluma ya Baraka shuleni Mkuu wa Shule ya Msingi Huruma Sr. Augusta Mlelwa amesema tangu alipoanza masomo yake shuleni hapo Baraka amekua na maendeleo mazuri sana kitaaluma kwani muhula wa kwanza akiwa darasa la kwanza alishika nafasi ya kwanza darasani huku muhula wa pili akishika nafasi ya pili kati ya wanafunzi 59 waliofanya mtihani.

Mapema mwezi Disemba 2023 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Juma Haji Juma mara baada ya kupata taarifa za mtoto Baraka alimulekeza Afisa Ustawi wa Jamii Bw. Filbert Mahay kumtembelea mtoto huyo nyumbani kwao kijiji cha Ugogo kilichopo Kata ya Mikalanga ambapo baada ya kujionea hali halisi ikabainishwa hatua ya haraka ni kumuwezesha vifaa hivyo saidizi.

Imeandikwa na Salum Said

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit