• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

JITIHADA ZACHUKULIWA KUTOKOMEZA UTAPIAMLO NA UDUMAVU MBINGA

Tarehe ya kuwekwa: March 31st, 2021

Imeandikwa na:

Salum Said,

Afisa Habari,

HALMASHAURI YA WILAYA YA MBINGA.

 

Wananchi wa Wilaya ya Mbinga wametakiwa kuzingatia ulaji unaofaa na unaojumuisha makundi matano muhimu ya vyakula na matumizi ya mbolea za asili ikiwa ni jitihada za kutokomeza tatizo la udumavu na utapiamlo mkali Wilayani humo.

Hayo yamebainishwa leo Machi 31 wakati wa kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kilicholenga kujadili hali ya lishe ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwa kipindi cha kuanzia Oktoba hadi Machi 2020/2021 kilichofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Kiamili na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali ngazi ya Wilaya, Kata, mashirika yasiyo ya kiresikali, viongozi wa dini na wadau wengine wa lishe.

Katika kikao hicho cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kilichoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Mhe. Cosmas Nshenye imeelezwa kuwa takribani 2% ya watoto waliopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga wana udumavu na utapiamlo mkali huku 98% ya watoto wakiwa na hali nzuri ya lishe, ushauri ukitolewa juu ya ulaji wa vyakula unaozingatia makundi matano ambayo ni wanga, protini, mbogamboga, mafuta na sukari hasa ya asili, na matunda mchanganyiko sambamba na udhibiti wa matumizi ya mbolea za viwandani ikiwa ni hatua muhimu na madhubuti katika mapambano dhidi ya udumavu na utapiamlo mkali Wilayani humo.

Akizungumza wakati wa Tathmini hiyo Mhe. Nshenye ametoa wito kwa viongozi wote wa ngazi ya Wilaya, Kata na Vijiji, wadau mbalimbali na wananchi kushirikiana kwa pamoja ili kuwa na jamii yenye uwezo wa kutoa maamuzi juu ya suala la lishe na kwamba kwa sasa ni vema jamii ikaelimishwa juu ya matumizi ya mbolea za asili (mboji na samadi) na kushirikishwa kwa ukaribu zaidi kwa maafisa ugani na idara ya kilimo katika jitihada za kupunguza matumizi ya mbolea za viwandani, lakini pia kuongeza matumizi ya chokaa kama ilivyopendekezwa na tafiti mbalimbali za hali ya udongo zilizofanyika Wilayani Mbinga.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Bw. Juma Mnwele amesema ataendelea kusimamia uwajibikaji wa kila mmoja na kwamba hatosita kuwachukulia hatua ikiwa ni pamoja na kuwabadilisha vituo vya kazi wale wote watakaoonekana kusuasua katika mapambano dhidi ya utapiamlo na udumavu na kuboresha hali ya lishe kwenye maeneo yao suala ambalo pia linatekelezwa kitaifa kote nchini.

Kwa upande wao wajumbe waliohudhuria kikao hicho wamesema wao kama wadau muhimu tathmini hiyo imewapata fursa ya kujipima na kuona walipotoka, walipo na wapi wanaelekea katika mkakati wa kutokomeza hali ya udumavu na utapiamlo nchini na kuahidi kushirikiana kwa pamoja kufanyia kazi mapungufu na changamoto zote zilizobainishwa wakati wa kikao hicho.

Kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kimefanyika hufanyika kila robo kufuatia kusainiwa kwa mkataba huo kuanzia ngazi ya Taifa, Mkoa, Wilaya, Halmashauri, Kata na Vijiji lengo likiwa kufanya suala la lishe kuwa mtambuka sio la Idara na Wizara ya Afya pekee na kwamba ushiriano wa pamoja unahitajika ili kutoa huduma za lishe kwa jamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit