• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

KIONGOZI MWENGE MAALUM ARIDHISHWA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI MBINGA

Tarehe ya kuwekwa: September 4th, 2021

Kiongozi wa Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru mwaka huu 2021 Lt. Josephine Mwampashe ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwa usimamizi na utekelezaji mzuri wa miradi yote ya maendeleo iliyotembelewa na Mwenge huo.

Luteni Mwampashe ametoa pongezi hizo leo Septemba 4, 2021 baada ya kuridhishwa na hali ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ambayo amesema ni matokeo ya usimamizi mzuri kufuatia  Mwenge wa Uhuru uliowasili mapema leo hii Wilayani Mbinga kukagua, kutembelea, kuweka jiwe la msingi na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

Mradi wa kwanza ambao umekaguliwa na Kiongozi wa Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru mwaka huu ni Klabu wa Wapinga Rushwa katika Shule ya Sekondari ya wasichana Mbinga (Mbinga Girls) Klabu ambayo awali ilizinduliwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru  mwaka 2018 yenye jumla ya wanachama 16 ambapo amepongeza uendelevu wa mradi huo.

Miradi mingine ni Jengo la Uthibiti Ubora wa Elimu lenye thamani ya Tshs. Milioni 181.8 ambalo limezinduliwa, Ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri iliyowekwa jiwe la Msingi, mradi ambao hadi kukamilika kwake utagharimu Tshs. Milioni 500 katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wake unaotarajiwa kukamilika Disemba mwaka huu 2021.

Katika hatua nyingine Kiongozi wa Mbio Maalum za Mwenge Lt. Josephine Mwampashe amekagua Kikundi cha Vijana cha Chipukizi kinachojishughulisha na ufyatuaji wa tofali za zege ambacho pia ni moja kati ya vikundi vilivyowezeshwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kupitia mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri hiyo kwa kupatiwa mkopo wa Tshs. Milioni 22 kwa mwaka wa fedha 2020/2021

Mwenge wa Uhuru umekimbizwa Wilayani Mbinga baada ya kupokelewa kijiji cha Mkako ukitokea Wilaya ya Namtumbo na unatarajiwa kukabidhiwa kesho Septemba 5 Wilayani Nyasa katika Kijiji cha Mkalole ambapo ukiwa Wilayani Mbinga umetembelea jumla ya miradi nane yenye thamani ya Tshs. Bilioni 3.14 kutoka Halmashauri zote mbili za Wilaya na Mji wa Mbinga.

Miradi mingine minne iliyopitiwa na Mwenge wa Uhuru kutoka Halmashauri ya Mji wa Mbinga ni Mradi wa Maji, Redio Hekima FM, Nyumba ya Mkurugenzi wa Mji pamoja na mradi wa Barabara ya Lami inayotekelezwa na Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini TARURA Wilaya ya Mbinga.

Imeandikwa na 

Salum Said,

Afisa Habari, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga 

4 Septemba 2021


Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit