Na Silvia Ernest, Mbinga DC
Katika kuhakikisha kuwa Halmashauri ya Wilaya ya mbinga inatokomeza kabisa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele hususan Usubi, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwa kushirikiana na Wizara ya Afya imeendelea kuongeza nguvu kila mwaka katika kampeni ya umezaji wa dawa kinga za Usubi kwa wananchi wanaoishi katika kata 29 za Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga.
Kauli hiyo inathibitishwa kitakwimu na ongezeko la idadi ya wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ambao wamejitokeza kumeza dawa za kinga tiba za Usubi mwaka 2023 ukilinganisha na mwaka uliopita yaani 2022.
Katika mwaka 2022 Halmashauri ilijiwekea lengo la kuwafikia wananchi 283, 531 na wananchi waliofikiwa ni 237, 249 sawa na 84% , kwa mwaka huu 2023 lengo lilikuwa kuwafikia wananchi 228,466 na wananchi 229, 414 walifikiwa ndani ya siku saba sawa na 100. 4%.
Takwimu hizo zinaonesha dhahiri kuwa jitihada zinazofanywa na Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga zinazaa matunda katika kuhakikisha ugonjwa huu wa Usubi na magonjwa mengineyo yaliyokuwa hayapewi kipaumbele yanatomezwa.
Mkuu wa Idara ya Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Dkt. Amad Mwalukunga alibainisha kuwa baada ya kubaini muitikio mdogo wa wananchi wa kumeza dawa za Kinga tiba za usubi kwa mwaka uliopita Halmashauri ilijiwekea mikakati ya kutatua changamoto hiyo.
Moja ya mkakati uliowekwa wa kuwafikia wananchi ni kufanya Mkutano na wananchi na kutoa elimu juu ya ugonjwa huo ili wananchi wapate uelewa wa kutosha wa dalili, madhara, kinga na tiba ya ugonjwa wa Usubi kabla ya kumeza dawa hizo.
Pili ni kuhakikisha wataalam waliopewa mafunzo kitaalam kutoka katika ngazi ya jamii wanapita kila Kaya/ nyumba kutoa dawa za Kinga tiba za Usubi ili kumfikia kila mwananchi na kuepusha usumbufu na gharama kwa wananchi kwenda katika vituo vya kutolea huduma za afya kumeza dawa hizo.
" Serikali iliona ni ngumu sana kwa wananchi kuja katika vituo vyetu vya kutolea huduma za afya na kupata hizi dawa kwahiyo mkakati tuliokuja nao ni kupita katika kila nyumba ili kuwafikia wananchi wote" Alisema Dkt. Mwalukunga
Aliongeza " Kabla ya kuwapatia dawa hizo tulitoa elimu ya kutosha ili kuondoa dhana potofu zinazosemwa na wanajamii kuhusu hizi dawa na kuwaelewesha wananchi juu ya madhara yanayoweza kupatikana kama hujameza dawa hizi"
Mwalukunga
alihitimisha kuwa mategemeo ya Halmashauri kwa mwaka ujao 2024 ni kuhakikisha kila mwananchi ambaye ana umri wa miaka kuanzia mitano ambae sio mjamzito au mgonjwa mahututi anafikiwa na zoezi la umezaji wa dawa za Kinga tiba za Usubi.
Mratibu wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Dkt.Joseph Washa Washa alibainisha kuwa magonjwa ambayo yalikuwa hayapewi kipaumbele hapo awali ni pamoja ugonjwa wa Usubi, Minyoo ya tumbo ,Kichocho , Matende na Mabusha pamoja na Trakoma.
Alieleza kuwa uelewa wa wananchi juu ya dalili, madhara pamoja na kinga ya magonjwa haya ni mdogo sana na pale mwananchi anapofika kugundua dalili tayari ugonjwa umeshaleta madhara makubwa.
" Kuna wananchi ambao wana ugonjwa wa usubi lakini hawajui kama wanao kwahiyo ni mhimu sana kuendelea kutoa elimu kwa wananchi ili sasa waelewe, na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga tunafanya hilo" Alisema Washawasha
Akizitaja dalili za ugonjwa wa Usubi ni ngozi kuwasha, ngozi kuwa na mabakamabaka kama ya kenge, uoni hafifu pamoja na upofu.
Bila kukwepesha Washa washa alibainisha kuwa madhara ya ugonjwa ya Usubi ni makubwa ikiwemo kuleta upofu, ngozi kuwa na madoa madoa kama ya chui pamoja kupoteza nguvu kazi katika shughuli za kiuchumi pindi mwananchi anapopata madhara tajwa.
Amethibitisha kuwa kinga na tiba za ugonjwa wa Usubi zipo, mwananchi anatakiwa kumeza dawa za kinga tiba ai…
MBINGA DISTRICT COUNCIL
Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA
Namba za simu: 2552640005
SImu ya mkononi: PS 0754533018
parua pepe: ded@mbingadc.go.tz
Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit