• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

MBINGA D.C YAFUNGUA MILANGO KWA WAWEKEZAJI

Tarehe ya kuwekwa: April 17th, 2021

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imeweka wazi milango ya uwekezaji kwa kutangaza fursa mbalimbali za kiuchumi zinazopatikana na kukaribisha watanzania kuchangamkia haraka fursa hizo kwa kuwekeza ndani ya Halmashauri hiyo.

Hayo yabebainishwa wakati wa kikao cha Baraza la Biashara la Wilaya kilichofanyika Mbinga Mjini Aprili 17, ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Juma Mnwele amesema Halmashauri hiyo ina utajiri wa fursa za kiuchumi na kutoa rai kwa mtu yeyote mwenye nia na dhamira ya kuwekeza basi kufanya hima kuja kuwekeza Mbinga.

Mkurugenzi huyo Mtendaji amebainisha kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ina maeneo mengi ya wazi, makubwa na mazuri ya uwekezaji kwa kufanyika shughuli na fursa mbalimbali kama Viwanda vya kusindika unga wenye virutubisho (Unga Lishe), vituo vya kuuzia mafuta (Petrol Stations), uchimbaji wa makaa ya mawe, uwekezaji kwenye kilimo cha mazao mbalimbali ya biashara kama parachichi, korosho, alizeti, soya, ufuta, na mengineyo ambayo kulingana na tafiti za hali ya udongo yanaelezwa kustawi vizuri kwenye maeneo mengi ndani ya Halmashauri hiyo.

Amesema anakaribisha na kuhamasisha wawekezaji kuja kwa wingi kuwekeza ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwani Halmashauri hiyo imeweka mazingira yote rafiki na salama kwa uwekezaji ikiwemo kurahisisha upatikanaji wa ardhi na maeneo ya uwekezaji pamoja na uwepo wa miundombinu na huduma muhimu kama umeme, maji na barabara huku akitolea mfano eneo la Kiamili na miji mingine midogo ya Maguu, Matiri, Kigonsera, Ruanda na Mkako ambayo tayari yameshapimwa na kutengwa maeneo maalumu kwa ajili ya uwekezaji.

Akizungumzia kuhusu fursa za uwekezaji zilizopo Kiamili, ambako ni Makao Makuu ya Halmashauri, Mkurugenzi Mnwele amesema kwa sasa Halmashauri hiyo inatekeleza mradi wa ujenzi wa jengo la Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji na ujenzi wa stendi ya mabasi na kwamba anatoa hamasa na kuwakaribisha wadau wa uwekezaji kuchangamkia fursa zilizopo ndani ya eneo hilo, akitolea mfano kuwekeza kwenye ujenzi wa vibanda zaidi ya 200 vya biashara vitakavyojengwa kuzunguka eneo la stendi kwa kuingia ubia na Halmashauri hiyo.  

Kikao cha Baraza la Biashara Wilayani Mbinga kimefanyika na kuongozwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Mhe. Cosmas Nshenye na kuhudhuriwa na viongozi, wafanya biashara na wadau wa biashara kutoka Halmashauri zote mbili za Wilaya ya Mbinga ambazo ni Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga na Halmashauri ya Mji wa Mbinga.

   

Imeandikwa na:

Salum Said

Afisa Habari

HALMASHAURI YA WILAYA YA MBINGA.  Aprili 17, 2021

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit