• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima

MBINGA DC YAONGOZA TENA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE

Tarehe ya kuwekwa: June 20th, 2022

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imeendelea kufanya vizuri katika utekelezaji wa mkataba wa lishe kwa kuwa na 128.22% ya utekelezaji wa viashiria vya lishe ikishika nafasi ya kwanza kati ya Halmashauri 8 za mkoa wa Ruvuma kwa kipindi cha robo ya tatu kuanzia Januari hadi Machi 2021/ 2022.

Akiwasilisha taarifa ya hali ya lishe wilayani Mbinga wakati wa kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mkataba na mapitio ya viashiria vya lishe vinavyofanyiwa kazi ngazi ya Halmashauri, Kata na Vijiji kilichofanyika Kiamili Jumatatu Juni 20, 2022 Afisa Lishe wa Halshauri ya Wilaya ya Mbinga Bi. Janeth Bandari amesema Halmashauri hiyo imeongoza katika utekelezaji wa viashiria vyote na kushika nafasi ya kwanza katika matokeo ya jumla ya utekelezaji wa afua za lishe huku Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo ikishika nafasi ya Pili.

Bi. Bandari amefafanua baadhi ya vigezo na viashiria vya lishe ambavyo Halmashauri hiyo imefanya vizuri kuwa ni pamoja na kufanyika kwa vikao vya lishe ngazi ya wilaya kwa kila robo mwaka, idadi ya watoto wenye utapiamlo mkali waliopatiwa matibabu, utoaji wa elimu ya ulishaji watoto wadogo na wachanga kwa wazazi na walezi, pamoja na uwepo wa taarifa za hali ya lishe zilizohuishwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

Ameongeza kuwa utekelezaji wa mkataba wa lishe katika robo ya 3 umefanyika kwa kuwapatia wazazi na walezi elimu ya ulishaji wa watoto wadogo na wachanga 9,991 kati ya 8,517 waliokusudiwa sawa na 117%, upimaji wa hali ya lishe kwa watoto 41,575 huku mtoto mmoja akibainika kuwa na utapiamlo mkali sawa na 0.002%, jumla ya wajawazito 8,202 walipatiwa nyongeza ya  vidonge vya kuongeza damu, utoaji wa elimu ya lishe katika shule za msingi na sekondari, uzinduzi wa  klabu za lishe  shule ya sekondari mkako pamoja na utoaji wa mafunzo kwa waratibu 58 walioko kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Lishe ya Wilaya ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Bi. Aziza Mangosongo amepongeza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwa kuendelea kufanya vizuri katika usimamizi na uboreshaji wa hali za lishe za wananchi wa Mbinga na kutoa wito kwa Afisa Lishe na Mganga Mkuu wa Wilaya kuhakikisha wanafanya ufuatiliaji wa maendeleo ya wale wote wanaobainika kuwa na hali mbaya ya lishe huku akisisitiza ulaji wa vyakula vyenye virutubisho vyote muhimu sambamba na kila mmoja kutenga muda wa kufanya mazoezi.

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imekua na mwendelezo wa kufanya vizuri katika utekelezaji wa mkataba wa lishe hadi ngazi ya chini ya kata na kijiji kwa mujibu wa afua na viashiria vyote vya lishe vilivyowekwa ambapo kwa kipindi cha robo zote tatu mfululizo kuanzia Julai hadi Machi 2021/2022 Halmashauri hiyo imeongoza kwa kushika nafasi ya kwanza kati ya Halmashauri zote 8 za Mkoa wa Ruvuma.

Na Salum Said, Juni 20, 2022 Kiamili-Mbinga.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAFUNZO KWA WALIOFAULU USAILI WA KAZI YA SENSA MBINGA DC July 27, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAOMBAJI WA KAZI YA SENSA 2022 NBINGA DC July 18, 2022
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI ENEO LA KIAMILI October 13, 2021
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MBINGA DC YAONGOZA TENA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE

    June 20, 2022
  • VIJANA FASTAFASTA WANUFAIKA MKOPO WA BAJAJI

    April 25, 2022
  • MIRADI 9 YATEMBELEWA NA MWENGE WA UHURU 2022

    April 10, 2022
  • KAMATI YA SIASA YARIDHISHWA NA UBORA WA MIRADI MBINGA DC

    March 18, 2022
  • Tazama zote/kote

Video

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mh. Christine Mndeme aagiza Halmashauri ya Wilaya kuhamiamia Kiamili kabla ya tarehe 30/10/2019
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Iringa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit