• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

"MBINGA HATUTAKIWI KUWA NA LISHE DUNI” - DC MBINGA

Tarehe ya kuwekwa: November 10th, 2022

Wananchi wa Wilaya ya Mbinga wameaswa kuzingatia ushauri na maelekezo ya wataalamu wa afya ya lishe juu ya ulaji unaofaa wa makundi mbalimbali ya chakula ili kukabiliana na uwepo wa wimbi kubwa la jamii yenye udumavu na utapiamlo mkali katika maeneo yao.

Wito huo umetolewa Alhamisi tarehe 10 Novemba 2022 na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Bi. Aziza Mangosongo wakati akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye maadhimisho ya Siku ya Afya ya Lishe kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga yaliyofanyika Kata ya Ngima, Tarafa ya Mkumbi.

Mhe. Mangosomo amesema wananchi wa Wilaya ya Mbinga na Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla ni wazalishaji wakubwa wa mazao ya chakula, huku mengi yakisafirishwa kwenda mikoa mbalimbali na nje ya nchi na kwamba ni aibu kubwa kwa wananchi hawa ambao Taifa linawategemea kwa usalama wa chakula kuendelea kukumbwa na tatizo la ukosefu wa lishe bora.

Mkuu huyo wa wilaya amesema ili kukabiliana na tatizo la lishe duni, udumavu na utapiamlo mkali jamii inatakiwa kuzingatia maelekezo ya wataalamu wa afya ya lishe juu ya ulaji bora wa chakula unaozingatia mlingano, mpangilio na uwiano sahihi wa makundi mbalimbali ya vyakula ili kuupatia mwili virutubisho vyote vinavyohitajika kwa ajili ya lishe na afya bora.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya amempongeza Mkurugenzi Mtendaji Juma Haji Juma, na uongozi mzima wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwa utekelezaji mzuri wa mkataba wa lishe kwa vitendo na kwamba anatambua namna ambavyo Halmashauri hiyo imekua ikitenga fedha za kutosha kila kwaka kwa ajili ya utekelezaji wa afua za lishe sambamba na usimamizi mzuri wa utekelezaji wa mikataba ya lishe kwenye vijiji na kata.

“Natambua Halmashauri hii inaongoza na ni kinara katika utengaji wa fedha na utekelezaji wa afua za lishe; nakuomba Mkurugenzi uendelee kuweka jitihada zaidi za kusimamia suala la lishe kuwa ajenda ya kudumu kwenye vikao vyote kuanzia ngazi ya kijiji, kata hadi huku wilayani” Amesema DC Mangosongo 

Awali akiwasilisha taarifa ya lishe mbele ya Mkuu wa Wilaya; Bi. Janeth Bandari ambaye ni Afisa Lishe wa Halmashauri amesema Halmashauri hiyo imeendelea kutekeleza muongozo wa kutenga shilingi 1,000/ kwa mtoto na kwamba mwaka huu wa fedha 2022/2023 jumla ya shilingi Milioni 92.7 zimetengwa kwa watoto 42,543 kwa ajili ya kutekeleza afua mbalimbali za lishe, sawa na wastani wa shilingi 2,179/ kwa kila mtoto.

Amesema hadi sasa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imefanikisha kutoa elimu ya ulishaji watoto wadogo na wachanga, kutoa vigonge vya madini chuma kwa akina mama wajawazito, matone ya nyongeza ya Vitamin A kwa watoto umri chini ya miaka 5 ambapo watoto wote 36,166 waliolengwa kwa kipindi cha kuanzia Julai hadi Agosti wamefikiwa. 

Maadhimisho haya ya Siku ya Afya ya Lishe yaliambatana na zoezi la upimaji wa hali ya lishe kwa jamii kwa kuangalia uwiano wa urefu na uzito, maonesho ya aina na makundi mbalimbali ya vyakula pamoja na mafunzo na elimu ya namna ya kuandaa uji wa lishe, unyweshaji uji na unyonyeshaji watoto wadogo na wachanga, na kwamba tayari kata 23 kati ya 29 za Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga zimeshafanya maadhimisho haya, sawa na asilimia 79.

Imeandaliwa na

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini 

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga 

Tarehe 10 Novemba, 2022

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit