Na Silvia Ernest
Shule ya Msingi Ndengu iliyopo Kijiji cha Likwela Kata ya Nyoni Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imepokea fedha kiasi cha shilingi 34, 555914.73 kwa ajili ya utekelezaji wa ujenzi wa matundu ya vyoo kupitia mradi wa School Wash Sanitation and Hygiene (SWASH).
Taarifa hiyo imetolewa na Afisa Elimu, Vifaa na Takwimu Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Ndg. Ambrose Ngonyani katika kikao cha kutambulisha mradi huo wa ujenzi wa matundu ya vyoo kilichofanyika katika Shule ya Msingi Ndengu tarehe 7 Desemba 2023.
Amesema kuwa Serikali kupitia mradi wa SWASH imetoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa matundu ya vyoo katika shule hiyo ili kuendelea kuboresha na kuimarisha miundombuni ya ujifunzaji na ufundishaji.
Aidha Ngonyani amewataka wajumbe hao kuhamasisha wananchi kwa Kijiji cha Likwela kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa mradi huo ili uwe mradi wa mfano kwa kukamilika ndani ya muda uliopangwa na katika ubora unaohitajika.
Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Nyoni Mhe. Kervin Kapinga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha hizo na kusisitiza kuwa atahamasisha wananchi katika kutekeleza mradi huo.
Naye Bw. Linus Nandera mwananchi wa Kata ya Nyoni amebainisha kuwa wananchi wa Kijiji cha Likwela wapo tayari kutekeleza mradi huo ambao utakwenda kuleta tija kwa wanafunzi wa Shule ya Ndengu.
MBINGA DISTRICT COUNCIL
Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA
Namba za simu: 2552640005
SImu ya mkononi: PS 0754533018
parua pepe: ded@mbingadc.go.tz
Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit