Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga limepitisha azimio la kumfukuza kazi mtumishi mmoja huku wengine watatu wakitakiwa kufunguliwa mashitaka ya kinidhamu kutokana na kukiuka maadili ya kiutumishi.
Maazimuzi hayo ya Baraza yamefikiwa tarehe 8 Februari 2022 wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani Robo ya Pili kujadili utendaji kazi wa Halmashauri kwa kipindi cha mwezi Oktoba hadi Desemba 2021/2022 uliofanyika kwenye ukumbi wa Shule ya Sekondari Kigonsera wilayani Mbinga Mkoa wa Ruvuma.
Akitangaza uamuzi wa mashauri ya kinidhamu na kiutumishi yaliyojadiliwa wakati Baraza lilipogeuka kuwa Kamati, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Mhe. Desderius Haule amemtaja mtumishi aliyefukuzwa kazi kuwa ni Godluck Gilbert Salim aliyekua Afisa Afya Mazingira wa Halmashauri hiyo.
Aidha, amewataja watumishi wengine ambao imeamriwa wafunguliwe mashtaka ya kinidhamu kutokana na utoro wa muda mrefu kwenye vituo vyao vya kazi kuwa ni Stella Christopher Mtuta (Afisa Mifugo Msaidizi), Dastan Zakaria Hyera (Mtendaji wa Kijiji) na Rafael Oswin Hyera (Mtendaji wa Kijiji).
“Baada ya Kamati kuwajadili kwa kutokuwepo kwenye vituo vyao vya kazi kwa muda mrefu wa zaidi ya siku 5; Kamati imeridhia na kufanya maamuzi kuwa watumishi hawa wafunguliwe mashitaka ya kinidhamu”. Amebainisha Mwenyekiti huyo wa Halmashauri.
Katika hatua nyingine, Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya MbingaBaraza limeridhia kuanza kwa mchakato wa kujaza nafasi wazi ya Mkuu wa Idara ya Fedha kwa kupitisha jina la Samwel James Marwa.
Imeandikwa na
Salum Said, Mbinga
Februari 8, 2022
MBINGA DISTRICT COUNCIL
Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA
Namba za simu: 2552640005
SImu ya mkononi: PS 0754533018
parua pepe: ded@mbingadc.go.tz
Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit