• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

RC RUVUMA ATOA RAI KILA MMOJA KUWAJIBIKA KATIKA UTUNZAJI WA VYANZO VYA MAJI

Tarehe ya kuwekwa: March 13th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amewataka wananchi na jamii ya Mkoa huo kuchukulia suala la utunzaji wa vyanzo vya maji kama sehemu ya utamaduni, desturi na utaratibu wa kawaida kwenye maisha yao ya kila siku.

RC Thomas ametoa wito huo leo Jumatatu tarehe 13 Machi, 2023 wakati wa hafla ya utoaji wa zawadi na motisha kwa wananchi na jumuiya zilizofanya vizuri katika kuhifadhi na kutunza vyanzo vya maji kwenye maeneo mbalimbali ya Wilaya za Mbinga na Nyasa Mkoani Ruvuma.

Katika hotuba yake kama Mgeni Rasmi kwenye hafla hiyo ambayo imefanyika kwenye ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Mbinga mjini leo Jumatatu tarehe 13 Machi 2023 Mkuu huyo wa Mkoa amesema utunzaji wa vyanzo vya maji ni jukumu la kila mmoja huku akisisitiza suala la upandaji wa miti na utunzaji wa miti hiyo ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

"Utunzaji wa vyanzo vya maji ni jukumu la kila mmoja wetu ikiwa ni pamoja na upandaji wa miti rafiki na kuhakikisha miti hiyo inalindwa na kutunzwa". Amesema RC Thomas.

Akitoa maelezo ya utangulizi kuhusiana na hafla hiyo ya kuwatunuku zawadi wananchi waliofanya vizuri katika utunzaji wa vyanzo vya maji Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Nyasa Mhandisi Elice Mnally amesema suala la zawadi ni utu lakini kutunza vyanzo vya maji ni wajibu wa kila mmoja na ni suala la maisha yetu, ustaarabu wetu na afya zetu kwa ujumla.

"Jitihada hizi tunazoziweka ni kwa sababu mkoa wa Ruvuma una vyanzo vingi vya maji na tuna wajibu wa kuhakikisha tunavitunza vyanzo hivi ili viweze kutusaidia kwenye maendeleo yetu ya kiuchumi lakini hata vizazi vinavyofuata." Amesisitiza Mhandisi Mnally.

Halfa hii imeandaliwa na Wizara ya Maji kupitia Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Nyasa na ni kufuatia ziara ya Waziri wa Maji Mhe. Juma Aweso mwaka 2022 alipotembelea miradi na vyanzo vya maji kwenye maeneo mbalimbali wilayani Mbinga na Nyasa na kuridhishwa na hali ya uhifadhi na utunzaji wa vyanzo hivyo ambapo alitoa ahadi ya kuchangia mifuko 150 ya saruji kwa ajili ya kuendeleza miradi ya maji ya jamii kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Halmashauri ya Mji Mbinga na Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa.

Imeandikwa na Salum Said 

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga 

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit