Na Silvia Ernest
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Yusuph Ismail ambaye pia ni Meneja Uthibiti na Ufuatiliaji wa Miradi REA amebainisha kuwa Serikali imetoa fedha kiasi cha shilingi Bilioni 28.8 kwa ajili ya kupeleka umeme katika Vijiji vyote ambavyo bado havijavikiwa na umeme vilivyopo katika Wilaya ya Mbinga.
Amefafanua kuwa katika fedha hizo Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imepata shilingi Bil.19.8 na Halmashauri ya Mji Mbinga imepata shilingi Bil.9.
Mhandisi Ismail amebainisha hayo Oktoba 9, 2023 katika ziara ya Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga ndani ya viunga vya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga.
Ameeleza kuwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga jumla ya Vijiji 74 ambavyo havikufikiwa na umeme vitafikiwa na umeme kabla ya Desemba 30, 2023 ambapo hadi kufikia leo Oktoba 9, 2023 tayari Vijiji 29 vimefikiwa na umeme huku Vijiji 45 vikiwa katika hatua ya utekelezaji.
Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Ndg. Juma Haji Juma ametoa wito kwa Wakala wa Nishati Vijijini ( REA ) kuimarisha usimamizi katika utekelezaji huo ili ukamilike kwa wakati na kuwanufaisha wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga.
Amesema" Tunaishukuru Serikali kwa kuona haja ya kuwafikia wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, tusimamie utekelezaji huu ilinukalete tija kwa wananchi hasa katika shughuli za kiuchumi"
MBINGA DISTRICT COUNCIL
Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA
Namba za simu: 2552640005
SImu ya mkononi: PS 0754533018
parua pepe: ded@mbingadc.go.tz
Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit