• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

TAKUKURU MBINGA YAENDESHA WARSHA UKUSANYAJI WA USHURU WA MAKAA YA MAWE

Tarehe ya kuwekwa: February 2nd, 2023

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Mbinga Alhamisi ya tarehe 2 Februari, 2023 imekutana na wadau mbalimbali wa makaa ya mawe kujadili changamoto na uwepo wa mazingira hatarishi na mianya ya rushwa katika mfumo wa ukusanyaji wa mapato yanayotokana na ushuru wa makaa ya mawe kwenye kizuizi cha kukusanyia ushuru huo cha Kitai.

Warsha hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Kigonsera, Mgeni Rasmi akiwa Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Bi. Aziza Mangosongo na kukutanisha wadau wa madini ya makaa ya mawe kutoka sekta za umma na binafsi wakijumuisha Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri, Kamati ya Usalama ya Wilaya, Maafisa Tarafa na Watendaji wote wa Kata na Vijiji.

Katika hotuba yake ya ufunguzi Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Bi. Aziza Mangosongo, ambaye alikua Mgeni Rasmi katika warsha hiyo pamoja na mambo mengine amesisitiza suala la uadilifu na uaminifu kwa watumishi wote wanaohusika na usimamizi na ukusanyaji wa mapato ya makaa ya mawe na mapato mengine ya serikali na kutoa wito kwa watu woye na mamlala zinazohusika kuendelea kuweka mikakati ya kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato.

Awali katika maelezo ya utangulizi kuhusiana na warsha hiyo Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Mbinga Frederick Msae amesema tukio hilo linafuatia zoezi uchambuzi wa mfumo wa ukusanyaji wa mapato yanayotokana na makaa ya mawe lilioendeshwa na ofisi yake kwa kipindi cha miezi michache iliyopita ambapo ufuatiliaji ulifanyika kuanzia eneo la mauzo ya makaa (sales points) kwa makampuni yote ya makaa ya mawe hadi eneo la ukaguzi na kukusanyia ushuru (check point) la Kitai.

Akibainisha zaidi juu ya kilichofanyika wakati wa ufuatiliaji wa mfumo wa mapato hayo yanayotokana na ushuru wa makaa ya mawe, Afisa wa TAKUKURU Blandina Hamisi ameeleza kwamba uchambuzi huo ulijikita katika maeneo kadhaa ambayo ni uzingatiaji wa Sheria ndogo za Halmashauri katika ukusanyaji wa ushuru wa makaa ya mawe na uwezekano wa kuwepo kwa mianya ya rushwa kwenye ukusanyaji wa ushuru huo.

Vilevile Ofisi hiyo ya TAKUKURU katika ufuatiliaji wake iliangalia changamoto na viashiria vinavyoweza kusababisha wakusanya mapato kwenye kizuizi cha Kitai kujiingiza kwenye vitendo na mazingira hatarishi na kupelekea upotevu wa mapato ambapo wajumbe waliweza kupitia na kujadili changamoto hizo, kuweka mikakati ya pamoja na hatimaye kupitisha maazimio kwa ajili ya utekelezaji.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ameishukuru Ofisi ya TAKUKURU kwa kubainisha changamoto kwenye ukusanyaji wa ushuru na mapato yatokanayo na makaa ya mawe na tayari Ofisi yake imeanza kuchukua jitihada mbalimbali ikiwemo kufungwa kwa kamera za CCTV na kuwekwa kwa mifumo ya umeme wa jua (solar system) na Tanesco kwenye kizuizi cha mapato cha Kitai na kuongeza kuwa ofisi yake ina mkakati wa kuweka kizuizi cha kisasa kitakachokua kinatumia kadi maalumu za kieletroniki kuruhusu gari za makaa ya mawe kupita (an electronic gate pass system).

Imeandikwa na Salum Said 

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini 

Tarehe 2 Februari, 2023

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit