Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ameipongeza timu ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwa kupata Kikombe 1 na Medali 7 katika mashindano ya Shirikisho la Michezo Serikali za Mitaa ( SHIMISEMITA) yaliyofanyika Jijini Dodoma kuanzia 18 hadi 31 Oktoba 2023, ameitaka timu hiyo kuongeza juhudi zaidi katika mashindano yajayo.
Mkurugenzi Juma ametoa pongezi hizo 2 Novemba 2023 alipozungumza na timu hiyo ofisini kwake mara baada ya timu hiyo kurejea Wilayani Mbinga kutoka Dodoma ilipokwenda kushiriki mashindano hayo.
Amesema " Niwapongeze sana kwa ushindi huu ila nitoe rai kwenye ushindi huu ukawe chachu kwenu katika kuleta ushindi zaidi"
Mwisho amemtaka Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Michezo na Utamaduni Ndg. Charles Maero kuongeza vipaji vingi pamoja na kuongeza muda wa mazoezi ili kuleta ushindi zaidi.
MBINGA DISTRICT COUNCIL
Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA
Namba za simu: 2552640005
SImu ya mkononi: PS 0754533018
parua pepe: ded@mbingadc.go.tz
Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit