• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

"UKIMWI BADO NI TISHIO" DC MANGOSONGO AONYA

Tarehe ya kuwekwa: December 1st, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mhe. Aziza Mangosongo amewataka wananchi wilayani humo kuwa na desturi ya kupima afya zao mara kwa mara na kuchukua hatua za kujikinga dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI ili kuunga mkono jitihada mbalimbali zinazochukuliwa na serikali katika kupambana na maambukizi ya virusi hivyo hatari duniani.

Akihutubia wananchi wakati wa maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambayo kwa Wilaya ya Mbinga yamefanyika Kata ya Mpepai Mhe. Mangosongo amesema jamii ikihamasika kwa wingi katika suala la upimaji wa Virusi vya UKIMWI (VVU) na kila mmoja akachukua hatua mara baada ya kutambua hali ya afya yake itasaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti kasi ya maambukizi ya virusi hivyo.

Mhe. Mangosongo ameongeza kuwa upimaji wa VVU ni jambo la hiyari lakini lenye umuhimu mkubwa na limekua likisaidia hata wale wanaobainika kuambukizwa VVU kuanzishiwa mara moja matumizi ya dawa za kufubaza makali ya virusi hivyo na kutoa wito kwa jamii kuweka UKIMWI na magonjwa mengine ya zinaa kuwa ajenda ya kudumu kwenye vikao, mikutano na mikusanyiko yote kuanzia ngazi ya vijiji na kata

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya ameongeza kuwa serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa afya imejipanga kuendelea kutoa elimu ya kinga dhidi ya VVU, elimu ya lishe na jinsi ya kuishi na VVU kwa waliombukizwa sambamba na utoaji wa elimu ya UKIMWI mahala pa kazi.

Awali akitoa taarifa kwa mgeni rasmi Bw. Andrew Kapinga, kwa niaba ya Mratibu wa Huduma za UKIMWI Kinga (DACC) Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga amesema hali ya maambukizi kwa Wilayani Mbinga kwa sasa ni asilimia 4 (4%) na kwamba jitihada mbalimbali zimekua zikichukuliwa katika mapambano dhidi ya VVU ikiwemo uhamasishaji wa tohara kwa wanaume, upimaji wa mara kwa mara na kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto

Bw. Kapinga amefafanua kuwa sababu zinazochangia ongezeko la maambukizi ya VVU kwa Wilaya ya Mbinga kuwa ni pamoja na kushamiri kwa ngono zembe, kurithi wajane na wagane, ulevi uliopindukia, umasikini miongoni mwa jamii na imani za kishirikina.

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani hufanyika tarehe Desemba Mosi ya kila mwaka, mwaka huu yakibebwa na kauli mbiu isemayo “Zingatia Usawa, Tokomeza UKIMWI, Tokomeza Magonjwa ya Mlipuko” ambapo kwa Wilaya ya Mbinga maadhimisho hayo yamefanyika Kata ya Mpepai, Halmashauri ya Mji wa Mbinga.

Imeandikwa na

Salum Said, Mbinga

1 Desemba 2021


Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit