• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

WANANCHI MBINGA NA FURSA ZITOKANAZO NA BIDHAA ZA MIANZI NA MISITU

Tarehe ya kuwekwa: March 29th, 2021

Wananchi wa Wilaya ya Mbinga wametakiwa kuchangamkia fursa mbalimbali zitokanazo na mianzi na bidhaa nyingine za misitu mara baada ya programu maalumu ya kuongeza mnyororo wa thamani mazao ya misitu kutekelezwa wilayani humo.

Hayo yamejiri baada ya Mkuu wa Wilaya yaMbinga na viongozi wengine wa Wilaya hiyo leo machi 29, 2021 kutembelea kikundi cha TUMEAMUA kilichopo Kata ya Ukata, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ambacho kinajishughulisha na ususi na uzalishaji wa bidhaa zitokanazo na mianzi.

Akizungumza na wanachama wa kikundi hicho Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mhe. Cosmas Nshenye ambaye pia aliambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, ametoa rai kwa kikundi hicho kuongeza aina na ubora wa bidhaa wanazotengeneza jambo litakalosaidia kukuza wigo wa soko na kuongeza thamani ya bidaa hizo.

Mhe. Nshenye ameongeza kwa kusema ni vema kwa kikundi hicho pamoja na vikundi vingine vinavyojishughulisha na ususi Wilayani Mbinga kubadilisha mtazamo wao na kuchukulia shughuli hiyo kama shughuli mojawapo na muhimu ya kiuchumi

Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya waliombatana na Mkuu wa Wilaya katika ziara hiyo wametoa wito kwa kikundi hicho kufikiria kuzalisha bidhaa nyingi zaidina tofautitofauti kama vitanda, viti, makochi, stiki za mishikaki, miko, vijiko na bidhaa nyingine za jikoni zitokanazo na mianzi badala ya bidhaa pekee zinazotengenezwa na kikundi kwa sasa ambazo ni ungo, makapu, majamanda, na mikoba.

Pia kamati hiyo imeshauri juu ya umuhimu wa kikundi kuwa na mchanganyiko wa wanachama hasa vijana na wanawake ili kuwa na muendelezo na kurithisha fani hiyo kizazi kijacho sambamba na kuruhusu na kukaribisha watu wenye fani tofauti kama mafundi seremala jambo litakalowezesha kuzalisha bidhaa za aina tiofauti na zenye ubora zaidi.

Akizungumzia juu ya ziara hiyo ya viongozi wa Wilaya kutembelea miradi inayofadhiliwa na programu ya FORVAC, Bw. Marcel Mtunda ambaye ni mratibu wa FORVAC kanda ya Ruvuma amesema lengo la ziara hiyo ni kushirikisha Serikali ya Wilaya kufahamu shughuli zinazofanywa na mradi na kutoa fursa kwa viongozi hao wa wilaya kujua maendeleo ya mradi kwa kila hatua inayoendelea

Bw. Mtunda ameongeza kuwa kupitia ziara hiyo viongozi wa Wilaya wameweza kutoa ushauri kwa watekelezaji wa mradi pamoja na wananchi juu ya nini kifanyike katika kuongeza thamani ya mnyororo wa mazao ya misitu, jambo litakalopelekea uendelevu wa shughuli za mradi mara muda wa utekelezaji wa mradi utakapofika kikomo

Kikundi cha TUMEAMUA ni kati ya vikundi 20 vinavyofadhiliwa na Programu ya Kuongeza Mnyororo wa Thamani Mazao ya Misitu FORVAC Wilayani Mbinga mradi unaofadhiliwa na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Serikali ya Finland ambavyo pamoja na ususi, vikundi vingine vinajishughulisha na ufugaji wa nyuki na biashara ya uyoga.

Imeandaliwa na:

Salum Said

Afisa Habari

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit