Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

WANANCHI MBINGA WATAKIWA KUEPUKA “MAJUNGU” WANAPOWASILISHA KERO ZAO

Tarehe ya kuwekwa: April 8th, 2021

Wananchi Wilayani Mbinga wameaswa kuzingatia ukweli, uwazi na kujiepusha na uonevu na ukandamizaji dhidi ya watu wasio na hatia huku wakitakiwa kufuata taratibu zilizopo wakati wa kuwasilisha malalamiko yao kwa viongozi.

Hayo yamebainishwa leo Aprili 8, na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Mbinga, Bw. Juma Mnwele aliyeambatana na Wakuu wote wa Idara na Vitengo wa Halmashauri hiyo wakati alipofanya ziara ya kutembelea Kijiji cha Kilindi kilichopo Kata ya Matiri na kuzungumza na wananchi kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika Kijijini hapo.

Ziara hiyo ya Viongozi wa Wilaya imefanyika kufuatia maagizo aliyoyatoa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bi. Christina Mndeme kwa viongozi hao wa Halmashauri kufuatilia ukweli na undani wa kero na malalamiko yaliyowasilishwa Ofisini kwake kupitia barua iliyoandikwa na baadhi ya wanaoelezwa kuwa wananchi wa Kijiji cha Kilindi, wakilalamikia Viongozi wa Kijiji hicho na Kata ya Matiri kwa ubadhirifu wa mali za umma sambamba na viongozi hao kujenga uhasama na chuki baina yao na baina ya wananchi.

Awali akifungua mjadala wa kupokea, kupitia na kutatua kero na malamiko mbalimbali kutoka kwa wananchi, Bw. Mnwele hiyo amesema wamekua wakipokea barua nyingi na zenye malalamiko mengi kutoka kijijini hapo na hivyo aliwataka wananchi kueleza kero na malalamiko yao kwa uwazi na kueleza kwa ukweli na kuepuka kuonea na kukandamiza viongozi ndani ya kata na watu wasio na hatia yoyote.

Baadhi ya wananchi waliozungumza kwenye mkutano huo wamesema hawaitambui barua hiyo iliyowasilishwa Mkoani wakieleza kusikitishwa kwao na jambo hilo, na kufafanua zaidi kuwa hakuna kikao wala mkutano waliokaa na kupitisha azimio la kuwasilisha barua ya malalamiko Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa ikiwemo pia kukana kujadili na kupitisha malalamiko yaliyopo kwenye barua hiyo.

Naye Diwani wa Kata ya Matiri Mhe. William Mbwambo amewataka wananchi kuacha ushabiki na uchochezi huku akisema barua hiyo imeandikwa na watu wachache ambao wamekua na tabia ya kupandikiza chuki kwa wananchi dhidi ya viongozi wa Kijiji na Kata hali inayopelekea kuzua taharuki na mvurugano kijijini hapo na kuongeza kuwa hata yeye binafsi amekua akiambiwa mambo mengi na watu hao ambayo hayana ukweli wowote.

Barua hiyo ya tarehe 3 Machi, 2021 imeelezwa kuandikwa na watu watano (5) waliojiorodhesha kwenye barua ambao ni Leo Komba, John Nchimbi, Kastrory Komba, Shaneli Kapusanga Komba na Elias Komba; wanne kati yao wakitokomea na kushindwa kuonekana kwenye mkutano huo huku mmoja (Elias Komba) akishangaa na kupinga vikali kushiriki kuandika barua hiyo na kusema siku ambayo barua inaelezwa kuandikwa alikua safarini.

Viongozi wa Halmsahauri ya Wilaya ya Mbinga mara kwa mara wamekua wakifanya ziara ya kutembelea vijiji na kata kwa kusudio la kukutana na kuzungumza na wananchi kupitia mikutano ya hadhara ili kusikiliza kero na malalamiko, kuona msingi wa malalamiko hayo na hatimaye kuyapatia ufumbuzi ili kuendana na misingi ya utawala bora katika kuhudumia wananchi.

Imeandikwa na:

Salum Said

Afisa Habari

HALMASHAURI YA WILAYA YA MBINGA. Aprili 8, 2021

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit