• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

WATANZANIA WAASWA KUJIWEKEA UTAMADUNI WA KUNYWA KAHAWA

Tarehe ya kuwekwa: October 1st, 2021

Watanzania wameaswa kuongeza hamasa na mwamko wa unywaji wa kahawa ili kuboresha afya zao sambamba na kuimarisha soko la ndani la zao hilo na hivyo kukuza uchumi wa wakulima na nchi wa ujumla.

Hayo yameelezwa leo Oktoba Mosi, 2021 na Bi. Mwanaidi Mang’uro ambaye ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbinga wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kahawa Duniani ambayo kwa Mkoa wa Ruvuma yamefanyika Kata ya Maguu Wilayani Mbinga na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa zao hilo kutoka Wilaya na Halmashauri zote za Mkoa wa Ruvuma.

Katika hotuba yake Bi. Mang’uro ambaye amemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kama Mgeni Rasmi kwenye maadhimisho hayo amesema pamoja na kuwa na uzalishaji mkubwa wa kahawa nzuri na yenye ubora Mkoani Ruvuma lakini bado kukosa utamaduni na utaratibu wa kunywa kahawa miongoni mwa wakulima, wadau na watanzania wengi ni moja ya changamoto zinazoirudisha nyuma sekta ya Kahawa nchini.

Aidha amesema kahawa ni zao la kiuchumi na tegemezi kwa Mkoa na nchi, hivyo utamaduni na desturi ya unywaji wa kahawa utaimarisha sana soko la ndani na kupunguza utegemezi kwenye soko la kimataifa kwani bei inapoyumba katika soko la dunia huathiri moja kwa moja pato na uchumi wa mkulima na Serikali kwa ujumla

Katibu Twala huyo ameongeza kuwa tafiti za kisayansi zinaonesha kuna faida nyingi za kimwili na kiafya za unywaji wa kahawa ikiwemo kuburudisha na kuchangamsha mtumiaji, kundoa sumu za vyakula mwilini lakini pia ikielezwa kuwa kahawa ni chanzo kikubwa cha madini ya Potassium, Phosphorus, Magnesium, Calcium na Sodium na hivyo kuchangia katika kuimarisha mifupa na ukuaji wa mwili.

“Kuna dhana ilisambaa miongoni mwa watanzania kuwa unywaji wa kahawa unasababisha maradhi ya moyo, presha, kisukari na kupelekea mtumiaji kukosa usingizi”. Amefafanua Mgeni Rasmi huyo huku akiwataka watanzania kupuuzia dhana na imani hizo potofu

Vilevile Bi. Mang’uro amewataka wakulima wa kahawa kwenye maeneo yote ya Mkoa wa Ruvuma kuzingatia kanuni bora za uzalishaji wa kahawa na kusisitiza matumizi ya mitambo ya kisasa ya kuchakata kahawa (CPU) ili kukidhi ubora na kuongeza thamani na bei ya zao hilo sokoni huku akionya kuepuka kuchakata kahawa majumbani.

“Lengo la Serikali ni kuona kahawa yote inayozalishwa inaandaliwa kwenye mitambo ya kisasa ya kuchakata kahawa ili kukidhi ubora na hatimaye iweze kuuzwa kwa bei nzuri”. Amesisitiza Katibu Tawala huyo.

Awali akizungumzia tukio hilo, Meneja wa Bodi ya Kahawa Mkoa wa Ruvuma Bw. Peter Buberwa amesema Maadhimisho ya Siku ya Kahawa Duniani hufanyika kila Oktoba Mosi ya kila mwaka na kwamba maadhimisho haya kwa mwaka huu yenye Kauli Mbiu isemayo ZALISHA KWA TIJA NA KUNYWA KAHAWA KWA AFYA yana lengo kuu la kuongeza hamasa ya unywaji wa kahawa nchini ambao upo chini kwa kiwango cha 7-10% ya uzalishaji na kuleta tija katika uzalishaji ambao bado upo chini kwa wastani wa robo kilo mpaka nusu kilo kwa mti wa kahawa.

Imeandikwa na

Salum Said, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga 

Oktoba 1, 2021


Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit