Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

WAZAZI WANAOLAZIMISHA WATOTO WAO “KUFELI” KUWAJIBISHWA

Tarehe ya kuwekwa: April 22nd, 2021

Wazazi na walezi Wilayani Mbinga wametakiwa kuwa chachu ya mabadiliko ya kukua kwa elimu na wale wote watakaobainika kuhujumu jitihada za serikali katika kukuza sekta ya elimu kwa kuhamasisha watoto wao kufanya vibaya kwa makusudi kwenye mitihani yao wamepewa onyo kali na kwamba hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Hayo yamebainishwa wakati wa kikao cha Tathmini ya Elimu Tarafa ya Mbuji kilichofanyika Aprili 22, ambapo baadhi ya wadau waliohudhuria kikao hicho wameibua hoja na mjadala kuhusu baadhi ya wazazi na walezi kuhujumu kwa makusudi jitihada za serikali katika kuboresha elimu kwa namna mbalimbali na kupelekea watoto kufanya vibaya kwenye mitihani yao ya mwisho licha ya wanafunzi hao kuwa na uwezo mzuri darasani.

Akizungumza kwenye kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Shule ya Mtakatifu Charles Borromeo, Kijiji cha Myau kata ya Mbuji na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa elimu, Afisa Elimu Mkoa wa Ruvuma, Emmanuel Kisongo amesema suala la usimamizi na ukuaji wa sekta ya elimu ni wajibu wa kila mmoja katika jamii nzima kuanzia ngazi ya familia na kwamba ni aibu kubwa kwa mzazi kulazimisha na kusababisha mtoto wake kufeli mtihani.

Bw. Kisongo amesisitiza kuwa jukumu la usimamizi wa elimu ni la kila mmoja na kwamba changamoto nyingi zilizotolewa kwenye kikao hicho zipo ndani ya uwezo wa jamii akitolea mfano utoro, mimba kwa wanafunzi, wazazi kutochangia chakula na mahitaji muhimu huku akitoa wito kwa jamii kuacha kulalamika na kutaka kila mmoja kekemea, kuchukua hatua na kuwajibika kulingana na nafasi yake.

“Wajibu wa usimamizi wa elimu ni wetu sote, hakuna kulalamika tuchape kazi na kukemea maovu hakuna mtu wa kukomboa watoto na jamii ya mbinga zaidi ya sisi wenyewe; tukiamua tunaweza” Amesema Bw. Kisongo. 

Imeelezwa kuwa baadhi ya wazazi wamekua wakiwapa vitisho watoto wao kwa kuwalazimisha kutoandika majibu sahihi kwenye mitihani, kuwatorosha watoto kipindi cha mitihani, kukwepa kutoa michango na mahitaji ya shule huku baadhi wakidaiwa kujihusisha na imani za kishirikina mashuleni na kupelekea wanafunzi kwenye shule hizo kushuka kitaaluma.

Awali akimkaribisha Mgeni Rasmi, Mwl. Samwel Komba ambaye ni Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ametoa taarifa kuwa hadi sasa jumla ya wanafunzi wanne (4) wamepata mimba, watatu kati yao wakiwa tayari wameshaandikishwa kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka huu na kukemea tabia ya baadhi ya wazazi na jamii kukwepa kutoa ushahidi na kesi nyingi kumalizwa nje ya mahakama na kuwataka kutoa ushirikiano kila wanapotakiwa kufanya hivyo.

Kikao cha Tathmini ya Elimu Tarafa ya Mbuji kimefanyika ikiwa ni mwendelezo wa vikao hivyo vinavyofanyika kwenye ngazi ya Tarafa ili kufanya tathmini ya hali ya ukuaji wa taaluma kwa kubainisha, kupitia na kujadili changamoto mbambali zinazoikabili sekta ya elimu na kuweka mikakati na maazimio ya pamoja yanayokusudia kuinua hali ya taaluma ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwa kushirikisha wadau wa elimu kama Madiwani, Watendaji wa Kata na Vijiji, Maafisa Elimu na wataalamu wengine ngazi ya kata na vijiji, wajumbe wa bodi na Kamati za Shule na wadau wengine muhimu.


Imeandikwa na:

Salum Said

Afisa Habari

HALMASHAURI YA WILAYA YA MBINGA.  Aprili 22, 2021

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit