• Wasilina nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mbinga District Council
Mbinga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • HISTORIA
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Afya
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maji
      • Community Development
      • Menejimenti ya Mipango na Takwimu
      • Mifugo
      • Agriculture,Cooperative and Irrigation
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
    • Kitengo
      • Habari, mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Investment
    • Makaa Ya Mawe
  • Huduma
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
  • Councillors/PM
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • UKURASA WA ELIMU SEKONDARI
    • Mbunge
      • Miradi iliyo inayofadhiliwa
      • Ratiba ya Mbunge
      • Ligi ya Mbunge
  • Miradi
    • Miradi
      • Miradi Mipya
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi ambayo haijakamilika
  • Chapisho
    • Miongozo
      • TEHAMA
    • Kanuni
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • TEHAMA
    • Idara
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Tarafa
    • Mbuji
      • KARIBUBU KATA YA MBUJI
      • Litembo
      • Kitura
      • Nyoni
      • Mpapa
      • Kata ya Kilangajuu
      • Maguu
      • Langiro
    • Kigonsera
      • Kigonsera
      • Kihangimahuka
      • Kitumbalomo
      • Matiri
    • Hagati
    • Mkumbi
    • Namswea
    • Mkumbi
      • Mkumbi
      • Kipololo
      • Ukata
      • Ngima
  • MIFUMO

WAZIRI WA ARDHI KUINGILIA KATI MGOGORO WA ARDHI “NDIKA”

Tarehe ya kuwekwa: April 29th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mhe. Cosmas Nshenye amewataka wananchi kuwa watulivu na wavumilivu wakati wanasuburi hatima ya mgogoro wa ardhi eneo la Ndika unaohusisha baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Mbinga wanaoendelea na shughuli za kilimo kwenye eneo hilo lililopo Wilayani Nyasa ambalo limepandwa miti.

Katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Mkuwani kati ya Mkuu huyo wa Wilaya ya Mbinga na wananchi wa vijiji vya Mkuwani na Mkuka uliofanyika leo aprili 30, Mhe. Nshenye pia ameonya wananchi kujiepusha na vitendo vya kihalifu na kutii sheria huku akiwataka kuwa watulivu hadi hapo mgogoro huo utakapopatiwa ufumbuzi na Waziri wa Ardhi.

Mhe. Nshenye ametoa wito kwa wananchi kufuata taratibu zilizopo pale inapotokea kutoridhishwa na maamuzi yoyote na kwamba sheria imewapa uhuru wa kupeleka malalamiko yao ngazi za juu huku akiwapongeza kwa hatua waliyochukua ya kuwasilisha malalamiko yao kwa Waziri mwenye dhamana na masuala ya ardhi.

Wakizungumza mbele ya Mkuu huyo wa Wilaya, baadhi ya wananchi wamelalamikia kunyanyaswa, kukamatwa na kutozwa faini wanapotembelea mazao yao ya chakula kwenye mashamba yaliyopo eneo la Ndika ambako wamekua wakifanya shughuli za kilimo kwa miaka mingi kabla ya uongozi wa Wilaya ya Nyasa kuanzisha mradi wa kilimo cha miti kwenye eneo hilo ikiwa ni mkakati wa Wilaya hiyo kuhifadhi mazingira ya eneo hilo lililopo kandokando ya Ziwa Nyasa.

Mgororo huo umefikishwa kwa Waziri wa Ardhi na baadhi ya wananchi kutoka kata za Kipapa na Maguu wanaoendelea na shughuli za kilimo kwenye eneo hilo la Ndika wakilalamikia kutoshirikishwa kwenye mchakato wa kubadilisha matumizi ya ardhi hiyo kwa kupanda miti na kwamba hawakubaliani na mpango huo kwa kuwa hawana maeneo mengine ya kulima mazao ya chakula.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Juma Mnwele akizungumza kwenye mkutano huo amewahakikishia wananchi wa vijiji hivyo kuwa viongozi wa Halmashauri na Wilaya wamekua na nia ya dhati ya kushughulikia mgogoro huo na kwamba jitihada viongozi hao wamekua wakifanya kila jitihada kutafuta suluhu na ufumbuzi wa suala hilo ikiwa ni pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kuandaa na kutenga zaidi ya ekari 123 kama maeneo mbadala ya kilimo kwa wananchi wote ambao mashamba yao yemepandwa miti. 

Imeandikwa na:

Salum Said

Afisa Habari

HALMASHAURI YA WILAYA YA MBINGA.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI September 17, 2024
  • TANGAZO LA HESABU MBINGA DC July 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA NAFASI YA MKUSANYA USHURU January 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA- DEREVA NAFASI 2 January 25, 2024
  • Tazama zote/kote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI KASHUSHURA ATOA MSISITIZO MATUMIZI YA NISHATI SAFI SHULENI

    February 15, 2025
  • MAAFISA TUME WATEMBELEA MBINGA DC

    January 08, 2025
  • WAANDISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA ANGALIZO

    January 09, 2025
  • KASHUSHURA AWAPONGEZA WANANCHI UJENZI WA SHULE

    September 10, 2024
  • Tazama zote/kote

Video

UGAWAJI WA MKAA MBADALA
Video zaidi

Kurasa za haraka

  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Utumishi
  • Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Polisi Tanzania
  • Mamraka ya mapato Tanzania (TRA)

Waliotembelea tovuti

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ili kutufikia

Wasilina nasi

    MBINGA DISTRICT COUNCIL

    Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA

    Namba za simu: 2552640005

    SImu ya mkononi: PS 0754533018

    parua pepe: ded@mbingadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Mlalamikaji
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit