Mwanafunzi Happiness Wello anayesoma kidato cha kwanza shule ya Sekondari ya Wasichana Mbinga ni kati ya wanafunzi wawili waliopokea msaada wa vifaa vya shule kutoka kwa Kamati maalumu ya maandalizi ya sherehe za maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Wilaya ya Mbinga.
Katika tukio la kuwatembelea na kuzungumza nao ambalo limefanyika leo Alhamisi tarehe 2 Machi 2023 Kamati hiyo imekabidhi msaada wa vifaa vya shule pamoja na fedha tasilimu kwa wanafunzi hao wanaotokea kwenye familia duni na mazingira magumu ambapo mwanafuzi wa pili anasoma kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari Mndeme iliyopo Kata ya Amanimakolo.
Tukio hili ni mwendelezo wa matukio mbalimbali yanayoendelea kwa kipindi chote kuelekea kilele cha Siku ya Wanawake Machi 8 mara baada ya uzinduzi rasmi wa Wiki ya Mwanamke uliofanyika jana Jumatano Machi Mosi ambapo Mgeni Rasmi alikua Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mhe. Aziza Mangosongo.
Aidha uzinduzi huo uliambatana na matukio mbalimbali ikiwa ni pamoja na tukio la kugawa mablanketi 20 na mashuka 20 kwa ajili ya wodi inayohudumia kina mama wajawazito na wazazi kwenye hospitali ya Halmashauri ya Mji Mbinga (Mbuyula).
Imeandikwa na Salum Said
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, tarehe 2 Machi 2023
MBINGA DISTRICT COUNCIL
Sanduku la posta: P.O. BOX 194 MBINGA-RUVUMA
Namba za simu: 2552640005
SImu ya mkononi: PS 0754533018
parua pepe: ded@mbingadc.go.tz
Copyright ©2021 Mbinga District Council. All rights Reserved. Prepared by ICT - Unit